
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Msigwa amesema maboresho hayo yanahusisha sehemu ya kuchezea (pitch), ambayo inatarajiwa kufikia viwango vya kisasa ndani ya kipindi cha miezi sita.
Ameeleza kuwa lengo ni kuwa na uwanja wenye viwango vya kimataifa, sambamba na kuboresha maeneo mengine ikiwemo sehemu za wageni maalum (lounges), vyumba vya kubadilishia nguo, ubao wa matokeo pamoja na mwonekano wa jumla wa uwanja.
Aidha, ameomba radhi kwa mashabiki wa soka kwa kutoweza kuutumia uwanja huo katika dabi ya Kariakoo iliyopangwa kufanyika Mei 3, 2026.
Hata hivyo, amesisitiza kuwa baada ya maboresho kukamilika, uwanja huo utakuwa katika hali bora zaidi na utadumu kwa matumizi ya muda mrefu.
Tupe maoni yako



0 comments:
Post a Comment