ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, February 28, 2026

VIDEO:- VIJANA 336 WAHITIMU VETA MWANZA, WANAOUZA VITENDEA KAZI WAONYWA.

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Jumla ya vijana 336 kutoka Wilaya za Ilemela na Nyamagana mkoani Mwanza wamehitimu mafunzo ya stadi za maisha na ufundi stadi katika fani mbalimbali, na kukabidhiwa vifaa vya kuanzia kazi ili kuwawezesha kujiajiri na kujikwamua kiuchumi. Vijana hao wamehitimu Februari 27, 2026 katika VETA Mwanza, ambapo wamekabidhiwa vyeti baada ya kupatiwa mafunzo ya uselemala, uashi, uchomeleaji, ufundi bomba, aluminium, umeme wa magari na majumbani, ufundi magari na upishi. Aidha, walipata elimu ya stadi za maisha, biashara, fedha, ujasiriamali, usawa wa kijinsia pamoja na teknolojia na TEHAMA. Wahitimu hao ni sehemu ya vijana 400 walioandikishwa katika awamu ya pili ya mradi wa Vijana Elimu, Malezi na Ajira (VEMA) unaotekelezwa na Plan International mkoani Mwanza, kwa lengo la kuwawezesha vijana kutoka familia zisizojiweza kupata ujuzi wa kujiajiri au kuajiriwa. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Amiri Mkalipa, amewataka vijana hao kuendeleza ujuzi walioupata na kuvitunza vifaa walivyokabidhiwa. Ameonya kuwa yeyote atakayebainika kuuza vifaa hivyo atachukuliwa hatua za kisheria.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment