ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 27, 2026

RAIS DKT. SAMIA AKISHIRIKI MISA TAKATIFU YA KUAGA MWILI WA MWADHAMA POLYCARP KARDINALI PENGO

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisaini Kitabu cha Maombolezo kufuatia kifo cha Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo mara baada ya kuwasili katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu Jijini Dar es Salaam, tarehe 27 Februari, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na viongozi mbalimbali kwenye Misa Takatifu ya kumuombea na kumuaga Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Marehemu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu Jijini Dar es Salaam, tarehe 27 Februari, 2026.




Kengele ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph ililia kwa dakika kumi mfululizo, mara tu baada ya mwili wa Askofu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Hayati Polycarp Kardinali Pengo, kuwasili kanisani hapo.

Na haya ni mambo machache kumuhusu;

1. Jina lake halisi ni nani? Kuna watu wanadhani Mwadhama ni jina lake? Wengine wanadhani Polycarp ni cheo chake. Jina lake ni Polycarp Pengo. Kardinali ni cheo cha Kanisa, na Mwadhama ni kivumishi cha sifa, kama ambavyo Maaskofu huitwa Mhashamu au Mbunge kuitwa Mheshimiwa.

2. Kwanini neno Kardinali lipo katikati ya majina yake na sio mwanzoni? Kwanini hakuitwa Kardinali Polycarp Pengo, akaitwa Polycarp Kardinali Pengo? Kanisa Katoliki lina utaratibu wa majina. Utaratibu huo huitwa modus titulorum ama style of titulature kwa kingereza. Kwa Makardinali wote, neno Kardinali hukaa katikati ya majina yao. Ndiyo maana Kardinali mpya anaitwa Protase Kardinali Rugambwa. Hata Papa Leo XIV kabla ya kuwa Papa aliitwa Robert Kardinali Prevost.

3. Kardinali Pengo ni miongoni mwa Maaskofu wachache kutoka Tanzania waliowekwa wakfu na Papa mwenyewe. Alipoteuliwa kuwa Askofu wa Nachingwea, aliitwa Vatican na kuwekwa wakfu na Papa John Paul II January 6, mwaka 1984 katika Basilika Kuu la Mtakatifu Petro.

4. Watu wengi wanashangaa kumbe Pengo alikuwa msomi wa kiwango cha PhD? Mbona alikuwa hajiiti Dr? Jibu ni kwamba katika Kanisa Katoliki, vyeo vya kitaaluma havipewi kipaumbele kuliko vyeo vya kiroho. Kuna doctrine ya unyenyekevu (humility) ambayo inasisitiza watawa wasijikweze kwa vyeo vya kisomi, bali wajitambulishe kwa nafasi zao za kiroho (Askofu, Kardinali, Padre etc).

Kardinali Pengo alikuwa na PhD ya Moral Theology kutoka Chuo Kikuu kinachoheshimika sana duniani cha Lateran, lakini maisha yake yote hakuwahi kujiita Dokta. Na hata pale TEC karibu Maaskofu wote ni PhD lakini huwezi kusikia wakijiita Dokta. Ni kwa sababu ya doctrine of humility.

5. Kwanini hakuzikwa kijijini kwao Mwazye, Kalambo? Ukiwa Mkleri utazikwa kwa utaratibu wa Kanisa. Mkleri ni mtu aliyepokea sakramenti ya daraja Takatifu. Hata hivyo angeweza kuzikwa Jimbo Katoliki Lindi au Tunduru-Masasi alipokuwa Askofu wa kwanza wa jimbo hilo. Lakini alishajiandalia kaburi lake kule Pugu. Na alichagua Pugu kwa sababu maisha yake ya utume yamekua zaidi Dar kuliko mahali pengine. Na pia alitamani kuzikwa pamoja na Wamisionari wa kale waliozikwa Pugu.!

Chanzo:  Malisa GJ 



Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment