Mabao ya Azam FC yamefungwa na kiungo Feisal Salum Abdallah dakika ya tatu tu ya mchezo na mshambuliaji mpya, Jean-Jacques Ngita Kamanga raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), aliyesajiliwa dirisha dogo kutoka Aris Limassol ya Cyprus akitupia magoli mawili dakika ya 19 na 59.
Kwa ushindi huo, Azam FC wanafikisha pointi 22 katika mchezo wa 10 na kupanda kwa nafasi tatu hadi ya tano, wakati Mtibwa Sugar inabaki na pointi zake 21 za mechi 16 nafasi ya nne.
Tupe maoni yako

0 comments:
Post a Comment