ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, August 29, 2025

MGOMBEA MWENZA CCM, Dk. NCHIMBI ATUA MWANZA, KUANZA KAMPENI.


Mgombea mwenza CCM, Dk. Nchimbiatua Mwanza, kuanza kampeniMgombea mwenza wa urais CCM, Dk. Emmanuel Nchimbi amewasili mkoani Mwanza leo Agosti, 29 tayari kwa kuanza ziara ya kampeni ya Uchaguzi Mkuu.

Dk. Nchimbi amewasiri katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza majira ya saa 2 asubuhi na kupokelewa na viongozi mbalimbali wa chama.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Tume Huru ya Uchaguzi ( INEC) Dk. Nchimbi leo atafanya mkutano mdogo Kwimba na baadaye mkutano mkubwa Ilemela na Nyamagama.

Akizungumza baada ya kuwasili mkoani Mwanza, Dk. Nchimbi amesema: "Tupo tayari na timamu kuanza kampeni za kuipeperusha bendera ya chama. 

Amesema pia, timu yake ipo tayari kuitangaza na kuitekeleza Ilani ya CCM.

................. ..................

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Nyamagana, kupitia kwa Mwenyekiti wake Comrade Peter John Begga, @begamotabiluteteia kwa kushirikiana na Kamati ya Siasa ya Wilaya, kinapenda kuwataarifu na kuwaalika wanachama na wananchi wote kuwa ijumaa hii ya tarehe 29 Agosti 2025 kuanzia saa 4:00 asubuhi Mgombea Mwenza wa Urais kwa Tiketi ya CCM, Mheshimiwa Dkt. Emmanuel John Nchimbi atawasili jijini Mwanza. Mapokezi rasmi yatafanyika Kata ya Buhongwa, na baadaye kufuatiwa na Mkutano Mkubwa wa Hadara wa Uzinduzi wa Kampeni za Mkoa utakaofanyika katika Uwanja wa Furahisha. Tunawakaribisha: - Mabalozi na wajumbe wao - Viongozi wa CCM wa Matawi yote 105 - Viongozi wa Kata zote 18 - Jumuiya za CCM (UWT, Wazazi, na Vijana) - Wananchi wote wa Jiji la Mwanza na maeneo ya jirani - Makundi mbalimbali: bodaboda, machinga, mama/baba lishe, wakulima, wafanyakazi, wajasiriamali na makundi maalumu. Njoo usikilize sera za maendeleo – si kelele. #Kazi_iendelee ............................................ KAMA UNAHITAJI KUTENGENEZEWA TANGAZO PIGA SIMU NAMBA 0754074152 JINA ALBERT GEORGE SENGO

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment