ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, March 19, 2024

SAO HILL HUZALISHA MICHE MILIONI 5 YA MITI KILA MWAKA

 

Mhifadhi mkuu wa shamba la miti Sao Hill PCO Tebby Yoram alisema kuwa miche hiyo huoteshwa kwa ajili ya kupandwa katika shamba hilo na mingine kugaiwa wananchi,wadau na taasisi mbalimbali.
Baadhi ya miti ikivunwa katika shamba la miti Sao Hill wilaya ya Mufindi mkoani Iringa 
Mhifadhi mkuu wa shamba la miti Sao Hill PCO Tebby Yoram alisema kuwa miche hiyo huoteshwa kwa ajili ya kupandwa katika shamba hilo na mingine kugaiwa wananchi,wadau na taasisi mbalimbali.


Na Fredy Mgunda, Iringa.

SHAMBA la miti Sao Hill lililopo wilaya ya Mufindi mkoani Iringa huotesha miche milioni 5 ya miti kila mwaka katika bustani tatu zilizopo katika shamba hilo.


Akizungumza na waandishi wa habari Mhifadhi mkuu wa shamba la miti Sao Hill PCO Tebby Yoram alisema kuwa miche hiyo huoteshwa kwa ajili ya kupandwa katika shamba hilo na mingine kugaiwa wananchi,wadau na taasisi mbalimbali.


PCO Yoram alisema kuwa lengo la kubwa la kugawa miche hiyo ni kuendeleza uhifadhi wa misitu kwa wananchi na taasisi hizo kuendelea kupanda miti kwa wingi katika mashamba na kushiriki katika kuhifadhi shamba hilo.


Alisema kuwa kuelekea kilele cha siku ya upandaji miti kitaifa itakayofanyika katika wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro na uongozi wa shamba hilo umejipanga kupanda miti kwenye vyanzo vya maji vilivyopo katika shamba hilo.


PCO Yoram alisema kuwa wanapanda miti kwenye vyanzo vya maji kwa lengo la kuendelea kutunza vyanzo vya maji na shamba la miti Sao Hill hupanda hekta 2500 hadi hekta 300 kila mwaka.


Aidha PCO Yoram alisema kuwa licha ya kupanda miti mingi lakini shamba hilo huvunwa Laki 6 hadi 7 ujazo wa uvunaji wa mazao ya miti katika shamba hilo kwa kuvinufaisha viwanda 400 ambavyo hutumia malighafi za misitu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.