ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 1, 2024

MGOMBEA CCM AJITOSA KUCHUKUA FOMU KUWANIA NAFASI YA UDIWANI KATA YA MSANGANI



NA VICTOR MASANGU,KIBAHA 


Mgombea wa nafasi ya kiti cha udiwani kata ya Msangani  Ndg.Yohana Chongela kupitia chama cha mapinduzi (CCM) leo  amechukua fomu rasmi ya kuwania nafasi hiyo katika ofisi za serikali ya kata ya Msangani.

Mgombea huyo ambaye alisindikizwa na umati wa wanachama wa CCM,viongozi mbali mbali pamoja na wananchi kwa lengo la kwenda kushudia namna ya jinsi anavyokabidhiwa fomu hiyo ya kugombea.

 Yohana mara baada ya kuchukua fomu hiyo kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi alitoa pongezi zake za dhati kwa viongozi na wanachama wote kwa kumpa ushirikiano katika kipindi chote za hatua za awali.

Aidha mgombea huyo aliwashuru wale wote ambao wamejitokeza kwa wingi katika zoezi zima la uchukuaji wa fomu na kuwaomba wampe ushirikiano katika kuelekea uchaguzi huo.

"Kwa kweli niwashukuru sana viongozi wa chama changu cha mapinduzi,wanachama pamoja na wananchi wenzangu kwa kuonyesha upendo wenu na kujitokeza katika zoezi hili la uchukuaji wa fomu,"alisema Mgombe huyo.

Katika hatua nyingine aliwaomba wanachama na wananchi wote kuendelea kumpa ushirikiano wa kutosha katika kipindi chote cha maandalizi ya kufanyika kwa uchaguzi huo.


Mgombea huyo ameweza kusindikizwa na  viongozi mbali mbali  wa CCM, Wanachama na Wananchi wa  wakiongozwa na  Domotila Kondo Katibu wa  CCM Kata ya Msangani ambaye ndiye Mkurugenzi wa Uchaguzi wa CCM  Kata ya Msangani.

Viongozi wengine wa Chama ambao pia waliweza kumsindikiza mgombea huyo ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Kibaha mjini Mwajuma Nyamka pamoja na makada wengine.

Uchaguzi wa kujaza nafasi ya udiwani katika kata ya Msangani ambayo ilikuwa wazi kufuatia aliyekuwa diwani wa kata hiyo kufariki unatarajiwa kufanyika Machi 20 mwaka huu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.