ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, February 21, 2024

RAMADHANI BROTHERS KUTOKA TANZANIA WATWAA TAJI LA 'AMERICA GOT TALENT'


Wanasarakasi wawili kutoka Tanzania kwa jina Ramadhan Brothers wameibuka washindi katika mashindano ya American Got Talent kitengo cha fantacy league.


Wawili hao wanaoshirikisha Fadhili Ramadhan na Ibrahim Jobu, walishinda taji hilo Jumatatu usiku.


Waliwashinda wapinzani wao wakuu Pack Drumline, V. Unbeatable, Sainted na Musa Motha.

‘Tunaamini Maisha yetu yanabadilika kuanzia wakati huo’, Ramadhan alinukuliwa na jarida la US Today akisema. ‘’Ushindi huu una maana kubwa kwetu, tuna furaha sana isio na kifani’’.


Kwa mujibu wa US Today, ushindi huo wa tuzo ya AGT ni safari ya miaka miwili ya vijana hao wawili.


Ramadhani Brothers walipanga kufanya majaribio ya "AGT" Msimu wa 17, lakini Jobu hakuweza kupata visa yake ya kusafiri kwa wakati.


Kwa muda, wawili hao walionekana kwenye mfululizo kadhaa wa "Got Talent", ikijumuisha "Australia's Got Talent," "Got Talent España" na "Românii au talent," ambayo ilianzisha jukwaa lao la kwanza la "AGT" Msimu wa 18.


Katika shindano hilo Ramadhani Brothers waliwashangaza waamuzi kwa onyesho linalohusisha mwanasarakasi mmoja kusawazisha uzito wa mwili wa mwenzake kichwani huku wakipita seti tofauti.


Hatahivyo licha ya kuingia fainali kama wahitimu wakuu, walipoteza kwa mshindi wa Msimu wa 18 Adrian Stoica & Hurricane.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.