ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, January 8, 2024

RC KUNENGE ATEMA CHECHE AAGIZA WATOTO WOTE KUPELEKWA SHULE HATA KAMA HAWANA SARE

 VICTOR MASANGU/ PWANI

MKUU wa mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge amewagiza walimu wa shule za msingi na sekondari kuwapokea wanafunzi wote waliojiunga kidato cha kwanza na darasa la kwanza bila kujali changamoto  za ukosefu wa sare za shule badala yake watoe  muda wa kukamilisha  taratibu zote za kujiunga na masomo.

Kunenge ametoa Maagizo  hayo wakati alipotembelea baadhi ya shule za msingi na sekondari katika  halmashauri ya mji wa Kibaha na kuzungumza na baadhi ya  wanafunzi waliojiunga na muhula Mpya wa masomo wa mwaka 2024.


Nao baadhi ya walimu wameelezea namna  mwamko wa wanafunzi waliojiunga na muhula huo Mpya wa masomo huku wanafunzi wakiahidi kufanya vizuri katika masomo yao. FIDELIS HAULE ni Mkuu wa  shule ya sekondari Tumbi.

Nao baadhi ya wanafunzi wa wa shuke ya sekondari Tumbi na Kibaha  hawakusita kuzungumza ya moyoni. MOSES DAMAS NA LIBYA OMARY ni wanafunzi walio wawakilisha wenzao.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.