ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, January 3, 2024

MBUNGE KOKA APIGA JEKI YA VIFAA VYA MICHEZO MICHUANO YA KIBAFA VIJANA CUP

 


VICTOR MASANGU,KIBAHA


KATIKA kuunga mkono juhudi za Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kukuza sekta ya michezo Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka ametoa vifaa  vya michezo ikiwemo jezi 16 na mipira 20  kwa ajili ya michuano ya vijana wenye umri  chini ya miaka 25.


Akikabidhi msaada huo  kwa viongozi wa Chama cha soka Wilaya ya Kibaha (KIBAFA)  katibu wa  Mbunge wa Jimbo la Kibaha mji Method Mselewa  alibainisha  kwamba lengo kubwa la kutoa vifaa hivyo ni kutoa fursa kwa  kuonyesha vipaji na kukuza mchezo wa  soka.

Katika halfa hiyo ya makabidhiano ambayo  imehudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Kibafa,pamoja na baadhi ya viongozi wengine wa chama cha mapinduzi (CCM ) kwa lengo la kushuhudia utekelezaji wa ilani katika nyanja ya michezo


"Leo kwa niaba ya Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini tumekuja kukabidhi vifaa vya michezo kwa uongozi wa soka Wiaya ya Kibaha na tumetoa mipira 20 pamoja na jezi seti  16 ambazo zimegharimu kiasi cha shilingi milioni 3.5 na zitapewa timu ambazo zitashiriki katika michuano hiyo," alisema Mselewa.
Aliongeza kuwa lengo la Mbunge ni kuendea kusaidia vijana wa jimbo lake katika kuendeleza na kukuza michezo mbali mbali katika kata zote 14  ikiwemo mchezo wa soka kwa vijana  wa Jimbo lake la Kibaha mjini.

Mselewa katika hatua nyingine alisema kuwa michuano hiyo ambayo mdhamini wake mkuu ni  Mbunge na kwamba wataendelea kushirikiana bega kwa bega na viongozi wa mpira wa miguu ili kutimiza malengo ya michuano hiyo.

Pia katika hatua nyingine aliwahimiza wacheza na timu zote kuwa na nidhamu na kuzingatia sheria na taratibu zote za mashindano ikiwemo kuzingatia suala la kutozidisha umri.


Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Chama cha soka Wilaya ya Kibaha (KIBAFA) Robert Munisi  amempongeza Mbunge Koka kwa kuweza kuunga jitihada za serikali katika kukuza sekta ya michezo hususan kwa vijana katika jimbo lake.

"Kiukweli napenda kwa dhati kabisa kumshukuru Mbunge wa Jimbo la Kibaha kwa kuweza kusaidia sekta ya michezo na amesaidia vifaa hivi kwa lengo la kufanikisha michuano hii ya vijana wenye umri chini ya miaka 25,"alisema Munisi.

Naye Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mji  amesema kwamba kite do alichokifanya Mbunge ni moja kati ya utekelezaji wa ilani kwa vitendo katika nyanza  ya michezo husan kwa vijana.


Makamu Mwenyekiti wa Chama cha soka Wilaya ya Kibaha (KIBAFA) David Mramba  ambaye pia ni Katibu mwenezi wa Chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani alisema kwamba dhamira ya Mbunge ni kuendeleza vipaji kwa vijana hivyo ni vema kumuunga mkono kwa dhati.


Mashindano hayo yaliyopewa jina la Kibafa vijana Cup  yanatarajiwa  kuanza kutimua vumbi lake rasmi kuanzia Januari 6 mwaka huu katika kiwanja cha Mwendapole  kwa kuzishirikisha time  16 kutoka Jimbo la Kibaha mjini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.