ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, September 4, 2023

NACHINGWEA WATUMIA MATOFALI YA PILIPILI KUDHIBITI TEMBO

 

Afisa Mhifadhi Mkuu Mamlaka ya usimamizi wa wanyama pori Tanzania Kanda ya Kusini Mashariki Linus Ezekiel Chuwa akitoa maelezo namna ambavyo mbinu za tofari la pilipili linavyoweza kufanya kazi ya kuwafukuza Tembo
Afisa Mhifadhi Mkuu Mamlaka ya usimamizi wa wanyama pori Tanzania Kanda ya Kusini Mashariki Linus Ezekiel Chuwa akitoa maelezo namna ambavyo mbinu za tofari la pilipili linavyoweza kufanya kazi ya kuwafukuza Tembo
Afisa Mhifadhi Mkuu Mamlaka ya usimamizi wa wanyama pori Tanzania Kanda ya Kusini Mashariki Linus Ezekiel Chuwa akitoa maelezo namna ambavyo mbinu za tofari la pilipili linavyoweza kufanya kazi ya kuwafukuza Tembo


Na Fredy Mgunda, Nachingwea.


Serikali kupitia Taasisi ya TAWA imeendelea na jitihada za kutokomeza changamoto ya Tembo wanaovamia makazi na mashamba ya wananchi katika wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi ili kuisadia jamii kufanya shughuli za kiuchumi bila usumbufu wowote.


Akizungumza wakati wa mafunzo ya namna ya kukabiliana na Tembo kijijini Mkoka Ruponda wilaya ya Nachingwea, Afisa Mhifadhi Mkuu Mamlaka ya usimamizi wa wanyama pori Tanzania Kanda ya Kusini Mashariki Linus Ezekiel Chuwa alisema kuwa serikali imekuwa ikitoa elimu kwa kila uchwao namna ya kukabiliana na Tembo.

Chuwa alisema kuwa serikali imekuwa ikutumia mikakati ya muda mrefu katika kukabiliana na Tembo,TAWA kwa kushirikiaha na PAMC Foundation imetoa mafunzo ya namna yakukabiliana na wanyama hao kwa kwa kuweka uzio wenye mchanganyiko pilipili na mafuta machafu pamoja na matumizi ya ndege Nyuki, matumizi ya gari Maalum na tofali la pilipili.

Alisema kuwa kuwafundisha mbinu hizo zitasaidia wananchi kuwafukuza Tembo na kuepukana na madhara ambayo yamekuwa yanatokana na mnyama huyo.

Chuwa alisema kuwa mbinu ya kuchoma tofari lilitengenezwa na kwa kinyesi cha mnyama pamoja na pilipili kutasiadia kuwafukuza Tembo Kwa kuwa mnyama huyo hapendi harufu ya pilipili.


kwa upande wao wananchi wa kijiji hicho wanaishukuru serikali kwa jitihada na mikakati inayoendelea kuchukuliwa namna ya kudhibiti mnyama Tembo ili asilete madhara kwa jamii husika.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.