ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 10, 2023

MASHABIKI MWANZA WAUZUNGUMZIA USHINDI WA YANGA IKIITANDIKA MARUMO 2-0, SHABIKI WA SIMBA ATIA FORA

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Baada ya mchezo kumalizika Jembe Fm ikiwa kibanda umiza ikateta na mashabiki wa soka, kwenye mic Jacob Mlay wa Sports Ripoti ya Jembe Fm Mwanza. ............................................................................................ MAGOLI. Ni Aziz Ki, kiungo wa Yanga alianza kutupia bao la ufunguzi dakika ya 63 kwa shuti akiwa ndani ya 18. Pamoja na kuanguka Morrison hakukata tamaa baada ya kuchezewa faulo na kipa pamoja na beki wa Marumo alikomaa akiamka chapchap akapiga mahesabu kujua goli liko wapi bila kuangalia kwa macho na kupachika bao la pili dakika ya 90 ya mchezo mpira ukitamatika kwa wenyeji #Yanga Sc 2-0 #Marumo Gallants. Hii inamaanisha YANGA kwa hivi sasa imetanguliza mguu mmoja hatua ya fainali. #samiasuluhuhassan

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.