ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, February 8, 2023

WAWILI WANASWA NA JESHI LA POLISI VURUGU ZA MACHINGA MWANZA LEO

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

JESHI la polisi mkoani Mwanza linawashikilia vijana wawili ambao imeelezwa walikuwa vinara wa kuhamasisha maandamano na kupelekea vurugu katika maeneo ya Makoroboi, Nyerere Square na Lumumba wilayani Nyamagana mkoani Mwanza. Akitoa taarifa juu ya vurugu hizo kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Mwanza WILBRAD MUTAFUNGWA amesema jeshi hilo linaendea pia kuwafuatilia na kuwabaini kundi la vijana wadogo waliojichanganya na baadhi ya machinga waliofanya maandamano hayo. Amesema vurugu hizo zimepelekea madhara mbalimbali lakini si madhara ya kibinadamu ambapo mpaka sasa mitaa hiyo imedhibitiwa na hali ni shwari kwa muktadha wa usalama. AIDHA KAMANDA MUTAFUNGWA AMESEMA JESHI HILO LIMEJIPANGA KUHAKIKISHA KUWAKAMATA WALE WOTE WANAOTAKA KUJARIBU KUFANYA VURUGU YOYOTE #samiasuluhuhassan #mwanza #VuruguMwanza #VuruguMachingaMwanza

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.