ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, January 4, 2023

WENGI WALITEGEMEA HARMONIZE ANGETAMBULISHA MENEJA WAKE USIKU ULE NINI KILITOKEA?

 

NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Kwa siku za hivi karibuni bila shaka ulizisikia taarifa zilizozagaa zikisema baada ya kuachana na aliyekuwa Meneja wake lakini pia mpenzi wake Kajala Frida , Msanii wa Bongofleva Harmonize alitangaza kumtambulisha meneja wake mpya kama Suprise kwenye usiku wa Harmo-Night , show yake ya kufungia mwaka iliyofanyika siku usiku wa Christmas ya Disemba 2022. Pia kupitia insta story, Harmonize amefunguka kuutumia usiku huo pia kutambulisha wasanii wengine wapya kwenye lebo ya Konde Gang. Akaenda mbali zaidi kwa kudai kuwa ataitumia show yake ya Harmo Night 2022, kupima upendo na unafiki wa wasanii wenzie haswa aliofanya nao kazi ya pamoja na kuzalisha Hit songs. Meneja wa Harmonize ambaye pia ni CEO wa Jembe Media Limited inayomiliki kituo cha Jembe Fm, Dr. Sebastian Ndege al maarufu Jembe ni Jembe, amezungumza leo na Natty E wa kipindi cha Hit Zone kinachochapa mangoma ya kileo kinachoruka mchana majira ya saa 13:00 hadi 16:00

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.