ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, December 19, 2022

NEYMAR AMPONGEZA MESSI NA KUMKAUSHIA MBAPPE BAADA YA ARGENTINA KUSHINDA KOMBE LA DUNIA.


Neymar katika ujumbe mfupi kwenye mitandao ya kijamii, alimpongeza Lionel Messi kufuatia ushindi wake wa Kombe la Dunia nchini Qatar.

Messi aliongoza Argentina kutwaa Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza tangu 1986 kupitia mikwaju kali ya penalti dhidi ya Ufaransa. Ilikuwa ni mechi babu kubwa ambayo iliwakutanisha mafowadi nyota wa Paris Saint-Germain Kylian Mbappe na Messi ambao walionyesha umahiri wao kwenye fani y soka. 

Messi alifunga mabao mawili huku Mbappe akidaka hattrick na kulazimisha mchezo kwenda kwa mikwaju ya penalti ambapo Emi Martinez alifunga bao moja kwa kuokoa. 

Ujumbe wa Neymar kwa Messi Neymar alimpongeza Messi kwa ujumbe mfupi wa 'Hongera Kaka.' Lakini mashabiki walikuwa wepesi kugundua kwamba hakuandika ujumbe wa kumfariji Mbappe ambaye licha ya umahiri wake wa kufungamabo alishindwa kutetea taji lao usiku huo. 

Inakumbukwa kuwa Neymar na Mbappe walikuwa na vita vya ubabe vilivyoripotiwa jijini Paris mwanzoni mwa msimu. 

Nyota hao wawili walisemekana kuwa na kinyongo huku Mbappe akiripotiwa akishinikiza kuuzwa kwa Neymar Timu ya Brazil ya Neymar, iliondolewa kwenye Kombe la Dunia katika hatua ya robo fainali na Croatia licha ya kuwa moja ya timu zilizokuwa zinapigiwa upatu kushinda taji hilo. Iwapo wangeliishinda Croatia, Neymar angelimwenyana na Messi katika nusu fainali. 

Nyota hao watatu sasa wanatarajiwa kurejea Paris hivi karibuni wakati miamba hao wa Ufaransa wakiendelea na harakati zao za kuwania taji la kwanza kabisa la Ligi ya Mabingwa. 

Paris Saint-Germain sasa wanajivunia kuwa na mshindi wa Kombe la Dunia na mshindi wa pili wa Kombe la Dunia katika kikosi chao.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.