ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 25, 2022

ALIZWA BAADA YA MKEWE KUTOROKA NA PESA ZAKE MILIONI 28.1AKIWA NA MCHEPUKO.

Manit na wanawe wakiwa katika kituo cha polisi baada ya mkewe kutoroka na pesa zake. 

Furaha ya mwanamume nchini Thailand aliyetambulika kama Manit, kushinda bahati na sibu iligeuka na kuwa ndoto mbaya baada ya mkewe kuchukua pesa hizo na kutoroka na mpenziwe.

 Mwanamume huyo wa miaka 49 alichanganyikiwa na kuvunjika moyo baada ya mkewe mwenye umri wa miaka 45, Angkanarat, kutoroka na shilingi milioni 28.1. 

Kwa mujibu wa ripoti ya shirika la habari ya The Thaiger, Manit alikuwa ameshinda pesa hizo kujpitia bahati na sibu mnamo Novemba 1, na kuweka hela hizo katika akaunti ya benki ya mkewe. 

Manit alipiga ripoti kwa polisi, ila maafisa hao walisema hawangemsaidia kwani pesa hizo zilikuwa kwenye akaunti ya benki ya Angkanarat.

 Isitoshe, wawili hao hawakuwa wameoana kihalali, kwa sababu hawakuwa na cheti cha ndoa. 

Wawili hao wameishi pamoja kam mke na mume kwa miaka 26, na wana watoto watatu, ila Manit alisema hakujuwa kama mkewe alikuwa na mpango wa kando. 

Angkanarat aliaambia shirika la habari la Thai kwamba hana mpenzi mwingine, ila alimkimbia mumewe kwa sababu alichoka na malalamiko yao na ya mwanao wa kiume. 

Pia alisema kwamba alitaka kuwa mtawa na sehemu ya pesa hizo alipeana kama ufadhili katika mashirika tofauti za msaada. 

Baada ya kupata habari kwamba anasakwa na polisi kufuatia ripoti ya mumewe, mwanamke huyo alirejea nyumbani siku ya Jumapili, Novemba 20, ili kufafanua yaliyojiri. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.