ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, October 13, 2022

MKOA WA PWANI WAJIZATITI KUBORESHA SEKTA YA ELIMU KWA KUJEGA VITUO VYA WATOTO.


Afisa elimu wa Mkoa wa Pwani Sara Mlaki akizungumza na washiriki wa warsha hiyo hawapo pichani iliyofanyika Wilayani Kibaha.

 Na Victor Masangu, Pwani 

Serikali mkoani Pwani katika kuunga juhudi za Rais wa awamu ya sita Samia Suluhu Hassan kuboresha sekta ya elimu kuanzia ngazi za chini imejenga vituo vya utayari vipatavyo 36 katika halmashauri zote lengo ikiwa ni kuwapatia elimu watoto waliosahaulika kupata fursa ya elimu ngazi ya awali.


Hayo yamebainishwa na Afisa elimu wa Mkoa wa Pwani wakati wa kufungua warsha ya mpango maalumu kwa ajili ya kuwandaa watoto hao waweze kuandaliwa vizuri katika  elimu ya awali kabla awajajiunga na darasa la kwanza.

Aidha afisa elimu huyo alibainisha kwamba nia yao kubwa katika mpango huo wa utayari ni kuwajengea uwezo na mahalifa ya katika suala zima la kuweza kujua kusoma,Kuhesabu na kuandika kabla ya kuingia darasa la kwanza.


Pia aliongeza kuwa wameamua kuwakutanisha wadau mbali mbali wa elimu wakiwemo madiwani,watendaji kata,waratibu elimu,wakuu wa shule ili tuweze kuweka mpango wa kuboresha sekta ya elimu kwa watoto hao ambao walishindwa kupata fursa ya kupata elimu ya awali.


"Lengo letu ni kuanzisha vituo vya utayari katika halmashauri zetu tisa kwa ajili ya watoto wetu wa kuanzia miaka 5 hadi 9  ili waweze kupata elimu ya awali kabla ya kuanza kujiunga na darasa la kwanza na halmashauri zetu zinatupa ushirikiano katika kufanikisha Jambo hili"alibainisha Sara.

 Kadhalika alisema kuwa mpango huo ambao umeanzishwa na serikali utawasaidia watoto ambao wamekosa fursa ya kupata elimu kuweza kujifunza zaidi katika kusoma,kuhesabu na kuandika.

 
Kwa upande wake afisa elimu ya watu wazima katika halmashauri ya Wilaya ya Rufiji Hamisi Chikaula amebainisha mpango huo wa utayari wa kuanzia vituo utaweza kuwa mkombozi mkubwa wa kuwasaidia watoto kupata elimu iliyo bora kuanzia ngazi za chini.


Chikaula ambaye pia alikuwa ni mmoja wa wawezeshaji katika Warsha hiyo aliongeza kuwa katika mpango huo kila halmashauri inajenga vituo vinne ambavyo vitakuwa ni mkombozi mkubwa kwa watoto kupata elimu ya awali.


Kwa upande wake diwani wa kata ya mkuza Focus Bundala ambaye ameshiriki katika Warsha hiyo ameahidi kuyafanyia kazi mafunzo yote ambayo wameyapata katika suala zima la kuwahimiza wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao katika vituo hivyo.

Diwani wa kata ya Visiga Kambi Legeza aliipongeza serikali ya awamu ya sita kwa kuanzisha mpango huo wa kujenga vituo ambavyo vitatumika katika kuwasaidia watoto ambao walikosa nafasi katika elimu ya awali.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.