ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, October 31, 2022

MARAIS WATATA AFRIKA WALIODINDA KUACHIA UONGOZI, TATIZO NI NINI?

 

Picha za baadhi ya marais wa Afrika ambao wamekuwa uongozini kwa muda mrefu na wangali uongozini. 

Bara la Afrika lina viongozi ambao baadhi wametawala tangu mataifa yao kupata uhuru. Baadhi ya viongozi hawa wakitawala kwa takriban miaka 40. 

Marais hawa hudai kuwa ni msukumo wa raia wao kuwa waendelee kuwahudumia licha ya vilio vya wengi wa wapinzani ambao hulalamikia kunyanyaswa na kura zao kuibwa. 

Katika miaka ya hivi karibuni, baadhi ya marais hawa wameondolewa mamlakani lakini wengine wachache wamesalia. 

Hii ni orodha ya rais watano ambao wametawala kwa muda mrefu barani Afrika: 


1. Teodoro Obiang Nguema – miaka 42 Rais wa Guinea ya Ikweta Teodoro Obiang Nguema ndiye rais aliyeoongoza kwa miaka mingi zaidi duniani nab ado angali mamlakani. 

Amekuwa uongozini kwa miaka 42. Alichukua mamlaka mwaka 1979 baada ya kumpindua mjomba wake. Teodoro Obiang Nguema ambaye amekuwa rais wa Guinea ya Ikweta kwa miaka 42 sasa. 

 2. Paul Biya – miaka 39 Rais huyu wa miaka 89 ameiongoza Cameroon tangu mwaka 1982. Mwaka 2018, alichaguliwa kwa muhula mwingine wa miaka saba. Paul Biya amekuwa rais wa Cameroon tangu mwaka 1982. 


3. Denis Sassou Nguesso – miaka 37 Huyu ni rais wa Congo-Brazzaville. Rais Sassou Nguesso amekuwa ofisini kwa miaka 37 sasa. 

Kwanza alihudumu kuanzia 1979 hadi 1992 na kurejea 1997 baada ya kukamilika kwa vita nchini humo. Alichaguliwa tena mwa muhula mwingine wa miaka mitano katika uchaguzi wa 2021. Rais Denis Sassou Nguesso ameiongoza Congo Brazzaville kwa miaka 37 sasa. 



 4. Yoweri Museveni – miaka 35 Rais wa Uganda Yoweri Museveni amekuwa uongozini tangu mwaka wa 1986 aliposhinda vita vilivyomwondoa mamlakani Amin Dada na utawala wake wa kiimla. 

Alichaguliwa kwa muhula wake wa sita katika uchaguzi wa Januari 2021. 

Rais wa Uganda Yoweri Museveni. Amekuwa mamlakani tangu mwaka wa 1986. 

6. Isaias Afwerki – miaka 29 Rais pekee ambaye a,efahamika na raia wa Eritrea tangu taifa hilo kupata uhuru ni Isaias Afwerki. Amekuwa mamlakani tangu Aprili 1993 ambapo ameongoza kwa miaka 29 sasa. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.