ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, June 27, 2022

DC MOYO ATATUA MGOGORO WA KIJIJI CHA UFYAMBE NA WAWEKEZAJI WA ZAO LA PARACHICHI

 

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiongea na wananchi wakati wa kutatua mgogoro  wa ardhi wa zaidi ya hekari 110 uliokuwepo baina ya wawekezaji na wananchi wa Kijiji cha Ufyambe.

Mmoja ya wawekezaji akiongea na wananchi wakati wa kutatua mgogoro  wa ardhi wa zaidi ya hekari 110 uliokuwepo baina ya wawekezaji na wananchi wa Kijiji cha Ufyambe.Wawekezaji wakiongea na wananchi wakati wa kutatua mgogoro  wa ardhi wa zaidi ya hekari 110 uliokuwepo baina ya wawekezaji na wananchi wa Kijiji cha Ufyambe.Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiongea na wananchi wakati wa kutatua mgogoro  wa ardhi wa zaidi ya hekari 110 uliokuwepo baina ya wawekezaji na wananchi wa Kijiji cha Ufyambe.


Na Fredy Mgunda,Iringa.


MKUU wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo amefanikiwa kutatua mgogoro  wa ardhi wa zaidi ya hekari 110 uliokuwepo baina ya wawekezaji na wananchi wa Kijiji cha Ufyambe.

 

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara,mkuu wa wilaya Mohamed Hassan Moyo alisema kuwa alipokea malalamiko ya wananchi juu ya wawekezaji hao kuwa wamechukua eneo la ardhi bila ridhaa ya wananchi.

 

Moyo alisema kuwa kazi ya serikali ya wilaya ni kuhakikisha kuwa wanatatua changamoto za wananchi pamoja na kuwasimamia katika maendeleo hivyo jukumu alilofanya alitimiza kama ambavyo inatakiwa iwe.

 

Alisema kuwa kitendo cha kuwaweka ndani viongozi wa serikali ya kijiji cha Ufyambe kilikuwa kitendo cha kutaka kupata ushahidi wa nini kinaendelea kwenye mgogoro wa ardhi baina ya wananchi na wawekezaji.

 

Moyo alisema kuwa serikali lazima inafanye kazi kwa mjibu wa katiba na sheria za nchi katika kuwatumikia wananchi ndio maana wamefanikiwa kutatua mgogoro huo.

 

Alisema kuwa wawekezaji walikiuka baadhi ya mambo ambayo yalikuwa yanaenda kinyume na kanuni za uwekezaji wa ardhi ya Kijiji hivyo baada ya kubaini hilo wawekezaji walifuata sheria zote.

 

Moyo aliwataka wawekezaji wote ambao wapo na wanataka kuwekeza katika ardhi ya wilaya ya Iringa wanatakiwa kufuata taratibu na sheria za uwekezaji ili wasibuguziwe.

 

Alisema kuwa wananchi wanapaswa kuendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji waliopo katika maeneo mbalimbali wanayazunguka ili kupata faida ya uwepo wa wawekezaji kama ambavyo wawekezaji wamekuwa wakichangia maendeleo kwenye miradi mbalimbali ya ujirani mwema.

 

Aidha Moyo alisema kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan anawakaribisha wawekezaji na anawapenda wawekezaji lakini anataka wawekezaji wafuate taratibu, sheria,kanuni na Katiba ya nchi.

 

John Lemomo,Baton Nsemwa na mchungaji Metili walisema kuwa walifanya kosa walipofika kuwekeza katika hatua za awali na kupeleka mgogoro ambao umetatuliwa na Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo.

 

Walisema kuwa wanamshukuru mkuu wa wilaya ya Iringa kwa kuwakumbusha kufuata taratibu na sheria za uwekezaji ili kuepukana na migogoro baina yao na wananchi wa maeneo husika.

 

Waliongeza kuwa wapo tayari kuwekeza katika Kijiji cha Ufyambe na wataendelea kutoa elimu kwa wawekezaji wengine ambao wanania ya kuwekeza ili wafuate taratibu na sheria za uwekezaji zinavyotaka.

 

Nao baadhi ya wananchi walisema kuwa wanakaribisha tena wawekezaji hao na wafanye uwekezaji wao kwa kufuata taratibu na sheria za uwekezaji ili kuepukana na migogoro baina ya wananchi wa Kijiji cha Ufyambe.

 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.