ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 11, 2022

RC SENDIGA ATOA SIKU SABA KWA MKANDARASI PRIPAM KURUDIA UPYA UJENZI WA BARABARA YA ZIZILANG’OMBE NGEREWALA

 

Mkuu wa mkoa wa Iringa Queen Sendiga akiwa kwenye ukaguzi wa barabara zaTARURA manispaa ya Iringa
Barabara ambazo mkuu wa mkoa wa Iringa alikuwa analalamikia kuwa zimejengwa chini ya kiwango
Barabara ambazo mkuu wa mkoa wa Iringa alikuwa analalamikia kuwa zimejengwa chini ya kiwango

Mkuu wa mkoa wa Iringa Queen Sendiga akiwa kwenye ukaguzi wa barabara zaTARURA manispaa ya Iringa

 Na Fredy Mgunda, Iringa.

Mkuu wa mkoa wa Iringa ametoa siku saba kwa mkandarasi Pripam kurudia upya ujenzi wa barabara ya Zizilang’ombe Ngelewala kwa kujenga chini ya kiwango na kusababisha barabara hiyo kuweka nyufa mwezi mmoja tu toka kukamilika kwake.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua ujenzi wa barabara za TARURA Manispaa ya Iringa,mkuu wa mkoa Queen Sendiga alisema kuwa hawezi kufarahishwa hata kidogo akikuta barabara imejengwa chini ya kiwango tofauti na thamani ya fedha iliyotolewa kwa mkandarasi.

Sendiga alisema kuwa haiwezekani barabara nyingi za manispaa ya Iringa zimejengwa kwa kiwango kizuri ispokuwa baarabara ya Zizilang’ombe Kitasengwa kwa kuwa imeanza kupasuka mapema jambo ambalo linaashiria kuwa barabara hiyo imejengwa chini ya kiwango.

Aliwataka wataalam Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini wilaya ya Iringa kuhakikisha wanawasimamia vilivyo wakandarasi ambao wanakuwa wamepewa tenda za ujenzi wa barabara wanajenga kwa ubora unaotakiwa kulingana na thamani ya fedha ambayo imetolewa kutoka serikalini.

Sendiga alisema kuwa baada ya siku saba atafanya ziara kukagua barabara hiyo kama imejengwa kwa kiwango kinachotakiwa kulingana na f thamani ya fedha ambayo imetolewa na serikali la sivyo mkandarasi atachukuliwa hatua kali za kisheria.

“Sijaridhishwa na ujenzi wa barabara inayotoka Zizi la Ng'ombe kuelekea Ngelewala Manispaa ya Iringa.Nimetoa siku saba kwa mkandarasi kuijenga upya kwa gharama zake na katika ubora unaotakiwa.” Alisema Sendiga

Aliwaambia wataalam wa TARURA wilaya ya Iringa kufanya kazi kwa weredi unaotakiwa ili kuiondolea serikali sitofahamu inayokuwa inaendelea kwenye mitandao ya kijamii juu ya ubovu wa barabara zinazojengwa katika wilaya ya Iringa.

Sendiga alimalizia kwa kuwapongeza viongozi wa TARURA Iringa kwa kazi wanayoifanya isipokuwa mradi mmoja wa barabara ya Zizilang’ombe Ngelewala ambao umeweka doa la mkoa kwa video za nyufa za barabara hiyo kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

 

Kwa upande wake meneja wa TARURA mkoa wa Iringa Makori George Kisare alisema kuwa wameyapokea mawazo na maagizo yote ya mkuu wa mkoa na watayafanyia kazi haraka ipasavyo kama alivyo agiza.

Akizungumzia swala la kupasuka kwa barabara ya Zizilang’ombe Ngelewala alisema kuwa mkandarasi anawajibu wa kurudia kwa gharama zake kwa kuwa yeye ndio aliyefanya kosa hilo la kiufundi.

 

Alisema kuwa watahakikisha wanamsimamia ndani ya siku hizo saba anafanya marekebisho yanayotakiwa kwenye barabara hiyo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.