ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 17, 2022

JAPAN YAZIONA MELI ZA KIVITA ZIKIELEKEA UKRANE.


Meli nne kubwa za kivita za Urusi zimeonekana zikisafiri karibu na visiwa vya Japan vya Honshu na Hokkaido zikielekea Ulaya, Reuters inaripoti.


Picha zilizochapishwa na wizara ya ulinzi ya Japani zilionyesha kile kilichoonekana kama malori ya kijeshi ndani ya meli hizo Zilizokuwa zikipita.


Alipoulizwa iwapo huenda zilikuwa zinaelekea Ukraine, msemaji wa waziri wa ulinzi wa Japan aliambia Reuters, "inawezekana".


Operesheni ya kijeshi ya Urusi haijaenda kama ilivyopangwa hadi sasa, huku vifaa vya kijeshi vikiharibiwa kwa kiwango kikubwa kuliko ilivyotarajiwa, kulingana na wachambuzi wa kijeshi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.