ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, March 13, 2022

AUAWA UGOMVI WA KUGOMBEA CHENJI YA SHILINGI 400

 


DEREVA wa bajaji na mkazi wa Miyuji, jijini Dodoma mwenye umri wa miaka 22, ameuawa kwa kupigwa na kipande cha bomba la chuma nyuma ya shingo  kutokana na ugomvi uliotokea baada ya kununua sigara na muuzaji kumgomea kurudisha chenji yake Sh 400.


Kamanda ya Polisi, Mkoa wa Dodoma, Onesmo Lyanga alisema mauaji hayo yalifanyika Machi 3,  mwaka huu katika Mtaa wa Tofiki, Kata ya Viwanda I Dodoma Mjini baada ya kutoa Sh 500 na kununua sigara ya Sh 100.


Alisema mtuhumiwa wa mauaji hayo ana umri wa miaka 22 na mkazi wa Chinyoya. Kamanda Lyanga alisema mtuhumiwa huyo amekamatwa.


Katika tukio lingine mwanamke mwenye umri wa miaka 40 na mkazi wa Mtumba  ambaye ni mfanya usafi alikutwa mtaroni akiwa ameuawa baada ya kukabwa shingo na kubakwa. Polisi inaendelea kufuatilia tukio hilo la Machi 9, mwaka huu.


Wakati huo huo, polisi kwa kushirikiana na askari wanyamapori walifanya upekuzi kwenye nyumba ya kulala wageni ya Highway iliyopo Kata ya Mtera, Wilaya ya Mpwapwa na kufanikiwa kukamata pembe za ndovu vipande vinne vyenye uzito wa kilogramu 10.65 vyenye thamani ya Sh milioni 69.4.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.