ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 27, 2022

RAIS SAMIA AWATAJA WANAOMTULIZA UBONGO WAKE.

 

🖐🏾Heri ya kuzaliwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.
#ShikaNeno
#TendaNeno
#Kaziiendelee
#HappyBirthday Mhe. @samia_suluhu_hassan
.
.
.
#JEMBE™

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata keki kama ishara ya kusherehekea kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa leo tarehe 27 Januari, 2022 Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa wajukuu zake ndiyo tiba yake kuu pale kichwa chake kinapokuwa kimejaa kwa mambo mengi hasa akiwa Dar es Salaam.


Hayo ameyabainisha hii leo Januari 27, 2022, wakati akisherehekea siku yake ya kuzaliwa jijini Dodoma, ambapo ametimiza umri wa miaka 62.


"Ukiona kichwa kimejaa zaidi tiba yangu ni wajukuu, napiga tu simu nileteeni hao kwahiyo wanakuja kwa masaa kadhaa hasa nikiwa Dar es Salaam, piga kelele panda shuka, pigishwa mbio kwenye ngazi wakirudi wanakokaa basi ubongo umepumzika," amesema Rais Samia

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.