ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, August 10, 2021

KISA CHA KWANZA CHA KIRUSI CHA MARBURG CHAGUNDULIKA GUINEA.

 


Guinea imethibitisha kisa cha ugonjwa wa Marburg, ikiwa ni mara ya kwanza kwa kirusi hicho hatari kinachohusiana na Ebola kutokea Afrika Magharibi. 
 
Kama tu ilivyo kwa ugonjwa wa COVID-19, kirusi hicho kinatoka kwa mnyama na kuingia kwa binaadamu. Shirika la Afya Ulimwenguni - WHO limesema kirusi hicho kinabebwa na popo na kina kiwango cha vifo cha hadi asilimia 88, kilipatikana kwenye sampuli zilizochukuliwa kutoka kwa mgonjwa mmoja aliyefariki Agosti 2 katika eneo la kusini mwa Guinea la Gueckedou. 
 
Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika Matshidiso Moeti amesema uwezekano wa kirusi cha Marburg kusambaa hadi maeneo ya mbali una maana wanahitaji kukizuia mapema. 
 
Ugunduzi huo unakuja miezi miwili tu baada ya WHO kutangaza kumalizika kwa mripuko wa pili wa Ebola nchini Guinea, ambao ulianza mwaka jana na kuwauwa watu 12.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.