ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, December 5, 2019

CRDB YAKUTANA NA MAWAKALA WAKE MWANZA - 2020 KUJA NA MAPINDUZI MAPYA.


Benki ya CRDB imejipanga kuendelea kuwekeza zaidi katika huduma za kidigitali ili kutoa huduma bora zaidi kwa wateja wake, anasema Daniel Mbaga ambaye ni Meneja Mwandamizi Kitengo cha Huduma Wakala CRDB.
Meneja Mwandamizi Kitengo cha Huduma Wakala Daniel Mbaga akipiga darasa mawakala mkoa wa Mwanza katika mafunzo ya yaliyofanyika katika ukumbi mkubwa Rock City Mall jijini humo.
Sehemu ya kusanyiko hilo la mawakala mkoa wa Mwanza katika mafunzo ya yaliyofanyika katika ukumbi mkubwa Rock City Mall jijini humo.
Meneja Mwandamizi Kitengo cha Huduma Wakala Daniel Mbaga akipiga darasa mawakala mkoa wa Mwanza katika mafunzo ya yaliyofanyika katika ukumbi mkubwa Rock City Mall jijini humo.
Licha ya Mafunzo hayo kulenga kuwaongezea Mawakala hao ufanisi katika utoaji huduma kwa wateja, pia yamelenga kuisaidia Serikali kutimiza azma yake ya kusambaza huduma nchini hasa maeneo ya vijijini ambako humuza ka kibenki zinahitajika kwaajili ya kusukuma harakati za maendeleo.
Kwa umakini Sehemu ya kusanyiko hilo la mawakala mkoa wa Mwanza katika mafunzo ya yaliyofanyika katika ukumbi mkubwa Rock City Mall jijini humo.
Meneja Mwandamizi Kitengo cha Huduma Wakala Daniel Mbaga akipiga darasa mawakala mkoa wa Mwanza katika mafunzo ya yaliyofanyika katika ukumbi mkubwa Rock City Mall jijini humo.
"Leo tuko hapa kwaajili ya kuwapa mafunzo yatakayo waboresha kiutendaji kwakuwapa mbinu mbalimbali za kisasa, kumshawishi mteja kuzichangamkia huduma  zetu zenye manufaa" asema  Daniel Mbaga, Meneja Mwandamizi Kitengo cha Huduma Wakala
Engo moja wapo ya kusanyiko.
Darasa linaendelea.
Aidha Mawakala hawa wamefundishwa pia ni kwanini umakini unahitajika kwenye shughuli zao za utoaji huduma za kifedha, suala zima la kuhakikisha wanajikinga na dalili zote za utakatishaji fedha hususani pale linapojitokeza genge la watu lililopanga kuwaharibia mitaji yao.
Kwa kuwa Benki ya CRDB ndiyo Benki inayoongoza kuwa na mawakala wengi nchini, hivyo mafunzo hayo yamepangwa kwenye kalenda kuwa endelevu yakipangwa kuwafikia mawakala wote wa maeneo mbalimbali nchini Tanzania.
Erick Willy ni Mkuu wa kitengo cha Huduma za CRDB Wakala (kushoto) akimkabidhi cheti ch ushindi nafasi ya pili Bi. Rose Josepha Mnangu.
Erick Willy ni Mkuu wa kitengo cha Huduma za CRDB Wakala (kushoto) akimkabidhi cheti cha ushindi nafasi ya tatu Alphrick FGeneral Supplies .
“Ningependa kuwakumbusha kuwa Sasa mteja wetu anaweza kufanya malipo akiwa ofisini kwake kwa njia ya mtandao wa intaneti akatuma pesa kwa wateja wake ambao pengine ingebidi awapelekee au waje pale, CRDB itaendelea kuboresha na tayari imesha fanikiwa kuongeza huduma nyingine bora ya malipo kwa njia ya mtandao ili kutengeneza fursa mbalimbali za kibiashara kwa wateja wetu”, alisema Erick Willy ni Mkuu wa kitengo cha Huduma za CRDB Wakala




Erick Willy ni Mkuu wa kitengo cha Huduma za CRDB Wakala (kushoto) akimkabidhi cheti cha ushindi nafasi ya nane Inocent Thobias.

Picha ya pamoja Meza kuu na Mawakala washindi.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.