ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, October 25, 2019

BAINA YA CHUO KIKUU CHA IRINGA NA WANANCHI SABA WA KATA YA KIHESA

 Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akifurahia jambo na bi Mwaija Ngaga mara baada ya kufanikiwa kumaliza mgogoro wako
 Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiwa kwenye meza moja na walalamikiwa pamoja na walalamika wakati wa kutatua mgogoro
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela kwenye picha ya pamoja mara baada ya kumaliza kutatua mgogoro

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela amefanikiwa kutatua mgogoro wa ardhi baina ya wananchi saba dhidi ya chuo kikuu cha Iringa uliodumu toka mwaka 1992

Akizungumza kwenye ofisi za mkuu wa chuo hicho,Kasesela alisema kuwa amefanikiwa kuutatua mgogoro huo kutokana na kuzikutanisha pande mbili ambazo zilikuwa zinagombana kuhusu ardhi ya chuo hicho ilipochukuliwa mwaka 1992.

“Huu mgogoro ni wa miaka mingi na mimi nimeukuta hivyo leo nimefanikiwa kuumaliza kwa njia ya busara kabisa kitu ambacho pale zilizokuwa zinalalamika zimefikia muafaka” alisema Kasesela

Aidha Kasesela alisema kuwa wamefanikiwa kumaliza mgogoro kwa kuwatafutia kila mmoja kiwanja kimoja ili kufidia maeneo ambayo serikaliilikipatia chuo kikuu cha Iringa.

“Nimewaagiza uongozi wa chuo kuwa ikifika siku ya jumatatu waje ofisini kwangu ili wawalipe nauli zao hawa wananchi kwa kuwa wanawajibu kwa mujibu wa makubaliano yetu ambayo tulikuwa tumefikia kwenye kikao hiki” alisema Kasesela

“Kwa leo nimefalijika kuona familia hii imeamua kumaliza mgogoro huu ambao ulikuwa hauna afya katika harakati za kuleta maendeleo kwa wananchi hawa kwa kuwa walikuwa wanapoteza muda mwingi kupigania mgogoro huu” alisema Kasesela
Kwa upande wa waliokuwa wanalalamika wakiwakilishwa Mwaija Ngaga pamoja na Zuhura Balama walisema kuwa wamelidhishwa na maamuzi yaliyofikiwa na kumpongeza mkuu wa wilaya ya Iringa kwa kumaliza mgogoro huo.

“Kwa kweli mkuu wa wilaya tunaomba ufikishe salamu zetu kwa Rais kwa kuchagua viongozi kama nyie wenye maono ya kushughulikia kero za wananchi maana la sivyo tulipanga kwenda Dodoma kumuona Rais” walisema wazee hao

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.