ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 9, 2019

ZURA YATOA BEI MPYA ZA MAFUTA YA SASA.



Na Thabit Hamidu,Zanzibar.

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (ZURA) imefanya mabadiliko ya bei za mafuta ambazo zitaanza kutumika rasmi kuanzia Tarehe 10/07/2019.

Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano ZURA Khuzaimat Bakari kwa waandishi wa habari, Amsema kuwa bei za mafuta kwa mwezi wa Julai zimeshuka kutokana na kushuka kwa bei za bidhaa katika soko la dunia, gharama za usafirishaji pamoja na bima.

Amesema kuwa bei mpya ya mafuta ya Petroli sh.2,338 ambayo sawa na asilimia 1.59%, mafuta ya dizeli yatauzwa kwa bei sh.2,319 sawa na asilimia 0.42%.

Aidha amesema kuwa bei mpya ya mafuta ya taa ni sh.1,753 sawa na asilimia 0.075% na mafuta ya Banka yameshuka na itakuwa ni sh.2.145 sawa na asilimia 0.46%.

Hata hivyo Khuzaimat amesema kuwa bei hiyo ni halali ambazo zitaanza kutumika hapo kesho.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.