ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 26, 2019

TURUDISHE FARAJA KWA DJ STEVE B A.K.A DJ SKILLS

Ndugu yetu Dj STEVE B a.k.a Dj Skills anasumbuLiwa na Maradhi ya FIGO, leo tulienda kumjulia Hali' na tulipoingia katika chumba alicholazwa tukapiga Story sana, katikati ya Maongezi alisema, “Mtu ukiwa mzima ni jambo la kumshukuru Mungu sana”, hii ni kutokana na Situation anayopitia.

Steve anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila, natoa Taarifa kwa Marafiki, Wasanii na Wadau wote wa Muziki, wengi hawana TAARIFA, kama tunavyojua Maradhi ya FIGO ni aghali sana.

Sisi kama MaDj/ndugu/marafiki Wenzake tunaangalia Jinsi ya Kushirikiana na Wadau ku-Raise Fund ili kufanikisha aweze kupata Tiba sahihi nje ya nchi, kwani Familia imefika pahala wanahitaji Msaada wa hali na mali.

Wapo waliochangia Matibabu tutawashukuru sana kwa Majina na Tutapeana Taarifa zaidi jinsi ya Kumsaidia mwenzetu Matibabu yake. 

Kwa Mawasiliano Zaidi wasiliana na Kaka yake 0687536015 #RudishaFarajaKwaDjSteve

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.