ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, July 17, 2019

Tsh Milioni 125 zilizokusanywa na Wafugaji kusaidia kaya Masikini Ngorongoro



Zaidi ya Tsh. Milioni 125 zimekusanywa na Wafugaji katika tarafa ya Ngorongoro wakishirikiana na Viongozi wa kisiasa na Taasisi za umma na binafsi ambazo zitatumika kuimarisha vikundi vya kuweka akiba na kukopa (Vikoba ) ili kusaidia kaya masikini kujikwamua kiuchumi.

Edward Maura ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafugaji  wafugaji kutoka vijiji vya tarafa ya ngorongoro amesema kuwa  wamekutana na kuanza kuchanga zaidi ya Tsh. Milioni 100 huku wengine wakijitolea mbuzi ng’ombe na kondoo, wafikika hatua hiyo baada ya kuona kuwa hakuna sababu ya kusubiri misaada kutoka nje wakati wenyewe wanauwezo wa kutatua changamoto zao kwa kuunganisha nguvu pamoja.

William Ole Nasha ni Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia na Mbunge wa Ngorongoro  amesema kuwa hatua ya kusaidia vikundi hivyo itasaidia katika kupunguza umasikini kwa wafugaji hao kwa kutumia Vikoba ambavyo vimekua vikileta matokeo makubwa katika uchumi wa wananchi.

James Ole Millya ni Mbunge wa Simajiro amesema kuwa uwezweshaji wa kundi la wafugaji wanaoshi katika mamlaka hiyo utasaidia pia katika kuibua vyanzo vipya vya mapato mbali na mifugo na pia na pia kuona umuhimu wa kuhifadhi rasilimali za wanyamapori na mazingira.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.