ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 30, 2019

KAMPUNI I ya Jatu PLC yaendesha mafunzo kwa vijana 100,yawaasa kuacha kutegemea kuajiriwa

KAMPUNI I ya Jenga Afya Tokomeza Umaskini (Jatu PLC), imeendesha mafunzo kwa vijana 100 lengo likiwa ni kutokomeza umaskini kupitia rasilimali watu.

Meneja mkuu wa Jatu, Mohamed Simbano akizungumza wakati wa mafunzo hayo alisema mkakati wa taasisi yao ni kusaidia kuondoa kutu vichwani mwa vijana kwa kuacha kutegemea kuajiriwa na badala yake waangalie fursa zilizopo na kuweza kujiajiri.

“ Tukiwa hapa kwenye mafunzo, una diploma, degree weka pembeni kwa sababu hazina maana sana kama huna uwezo wa kubuni wazo na kutengeneza pesa,” alisema Simbano na kuongeza

“Aliyejaribu na akashindwa, anafaida kubwa kuliko asiyejaribu, kufeli haina maana umeshindwa bali utatafuta namna nyingine ya kujaribu.” Alisema

Akimnukuu mwanafalsafa Joseph Chilton Pearce aliyeelezea thamani ya ubunifu aliyosema, ‘to live a creative life we must lose our fear of being wrong’ kwa tafsiri isiyo rasmi alimanisha kuishi maisha ya ubunifu kunahitaji kuondoa hofu ya kukosea.

Simbano alisema elimu ambayo wanawapatia vijana hao itawaondoa katika dhana ya kusaka ajira au kubweteka majumbani na badala yake watachukua hatua na kujiikingiza kwenye ujasiriamali wa kilimo na masoko.Alisema mafunzo hayo ni bure kwa kila kijana mwenye ndoto za kujikwamua kiuchumi,bila kujali elimu.

Alisema mara baada ya mafunzo hayo watatoa nafasi kwa vijana katika masoko kwa kuwaajiri na kuimarisha kitengo chao cha masoko, hadi kufikia mwaka 2022 kila anayetumia soko bidhaa za Jatu aweze kupata manufaa na kwamba chakula kinacholiwa kiwe suluhisho la masoko.

“Mafunzo haya ni endelevu, vijana 100 tutakaowapa ajira ni fursa pekee kwao kwa kuimarisha kitengo cha masoko cha Jatu, na kazi yao kubwa ni kuhakikisha kila mwanachama wa jatu aweze kutumia bidhaa.” Alisema

Alisema mafunzo hayo yanaenda sambamba na mpango mkakati na kufikia malengo, waliojiwekea ikiwemo kutokomezaz umaskini kupitia rasilimali watu, kilimo na viwanda, ikiwa ni pamoja na kuingia kwenye soko la hisa (DSE) mwezi Septemba.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.