ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 29, 2019

MAN Utd YATHIBITISHA KUMSAJILI MLINZI WA Crystal Palace



Manchester United wamemsajiili beki wa Crystal Palace, Aaron Wan-Bissaka kwa mkataba wa pauni milioni 50.
Kiungo huyo wa miaka 21 amekubali kutia saini mkataba wa miaka mitano utakaomwezesha kulipwa hadi pauni 80,000 kwa wiki.
United tayari imelipa £45m kumnunua Wan-Bissaka amabye anatajwa kuwa mchezaji wa tano mkubwa kusainiw ana klabu hiyo baada yaPaul Pogba, Romelu Lukaku, Angel di Maria na Fred.
"Siamini nimejiunga na Ma Utd kwa kweli najivunia sana usajili huu," Wan-Bissaka alisema.
Manchester United imethibitisha usajili wake leo Jumamosi.
Kocha wa klabu hiyo Ole Gunnar Solskjaer amesema Wan-Bissaka ni "mmoja wa walinzi wakuu wanaoibuka katika ligi ya Premia".
Aliongeza kuwa: "Ana eshiku kazi yake, ana talanta kubwa inayomwezesha kuchezea Manchester United na ana vigezo vyote vya mchezaji tunayemtaka ajiunge na kikosi chetu na bila shaka atatusaidia kufikia malengo."
Mlinzi huyo ni ni wa pili kusajiliwa na klabu hiyo, baada ya usajili wa kiungo wa kimataifa wa Wales Daniel James, 21, ambao alijiunga na United kutoka Swansea kwa £15m.
United wana nafasi ya kurefusha mkataba wa miaka mitano wa Wan-Bissaka hadi miaka sita.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.