ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, March 5, 2019

MRISHO MPOTO AMLIZA MAKONDA, RIDHIWAN, MONGELLA, STEVE NYERERE, ADEN RAGE NA MAMA HUYU


BAADA ya kupasa sauti zaidi ya mara tatu akiliita jina la mja mwendazake Ruge Mutahaba, huku wengi wakihisi huenda kwa sauti yake hiyo marehemu angeweza kunyanyuka akiwa hai, akilia kwa uchungu mwanamuziki Mrisho Mpoto, ananena maneno haya.....

"Unasema tusilie, Umetuambia tusilie, Nani anaweza kuzuia machozi yasitiririke katika viwanja hivi Ruge? Naniiiiiiiiiiiiiii anyooshe mkono, anyanyue kidole aseme tusilie"


"Ikiwa Mungu ameweza kupokea maombi yetu ya kusimamisha mvua ili leo tukulilie, Tukushangilie kwa machozi, nauliza ni nani atakayemudu kututuliza...............?" 

Mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media, Ruge Mutahaba umezikwa kishujaa nyumbani kwao katika kijiji cha Kiziru Kata ya Karabagaine Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera huku mamia ya watu wakiwemo viongozi wa serikali wakishiriki mazishi hayo. 

Zoezi la kuzika mwili wa Ruge lilianza kwa Ibada ya mazishi ambayo iliongonzwa na Katibu wa Parokia ya Itahwa, Anatory Kyatwa huku nyimbo za maombolezo za kiswahili na za kabila la kihaya zikipamba tukio la mazishi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.