ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 16, 2019

BREAKING NEWS: WENYEVITI 7 CHADEMA WATIMKIA CCM.


Wenyeviti Saba wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo  ( CHADEMA )
Wilayani Arumeru mkoani Arusha wamejiunga na Chama cha Mapinduzi CCM mapema jana katika ziara ya kikazi ya Mkuu wa wilaya hiyo Ndugu Jerry Cornel Muro katika Kata ya Maji ya Chai , Wenyeviti wameamua kujiuzulu baada ya hapo juzi aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki Ndugu. Joshua Nassary kuvuliwa ubunge na Spika wa Bunge la Tanzania baada ya kutokuhudhuria vikao vitatu vya bunge mfululizo 


Dc Muro akiwa ameambatana na Katibu wa CCM Wilaya ya Meru Mwalimu Kanuthi wamewapokea wenyeviti hao walioleza kuwa wameamua kujiunga na CCM ili kumuuunga mkono Rais John Pombe Magufuli Kwa utendaji Kazi wake Sambamba na kumpongeza Mkuu wa Wilaya hiyo kwa kazi anazozifanya na namna anavyotatua migogoro ya wananchi  

Mwenyeviti waliopokelewa ni Mwenyekiti wa kijiji cha Ngurdoto Ndugu Mosses Ayo.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Maji ya Chai Ndugu Mase David Mbise pamoja na hapo amewapokea wenyeviti wa vitongoji vitano ambavyo ni Ndugu Perfect Philemon Mwenyekiti wa kitongoji cha Bondeni,Laurant Kessy Kitongoji cha Mburueshi, Elisante Akyoo Kitongoji cha KCenter Mwenyekiti wa kijiji cha Seneto Ndugu Christopher Mbise  pamoja na Ndugu Amani Kitali Mwenyekiti kitongoji cha Kimandafu

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.