ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, February 27, 2019

RUGE AMTOA MACHOZI MKUU WALIYE SOMA NAYE SHULE MOJA.


MKUU wa Mkoa wa Mwanza John Mongella amesema kuwa baada ya kupokea taarifa za msiba wa Ruge Mutahaba usiku wa jana hakuweza kupata usingizi kwa kuweweseka.

Mongella amesimulia mazito ya ukaribu wake na marehemu Ruge alioanzia shuleni hadi nyumbani kwa wazazi.

WAKATI HUO HUO.

Familia imeamua kwamba Ruge Mutahaba atakwenda kuzikwa nyumbani kwao huko Bukoba siku ya Jumatatu, siku ya Jumapili mwili utasafirishwa kwenda Bukoba.

Afya ya Ruge Mutahaba ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group (CMG) ilianza kutetereka katikati mwa 2018, na Juni mwaka huo alikwenda India kwa ajili ya matibabu na alirejea nchini Agosti 21, 2018.

Baada ya muda kidogo hakuonekana, Oktoba 2018 alipelekwa Afrika Kusini kwa matibabu, amekaa huko hadi alipofariki.

Ruge Mutahaba amefariki siku ya jana nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu ya figo. Ruge alizaliwa mwaka 1970, Brooklyn nchini Marekani, atakumbukwa zaidi kwa mchango wake mkubwa katika sekta ya muziki nchini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.