ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 23, 2018

SERIKALI KUJENGA VITUO VYA POLISI 65 KATIKAWILAYA MPYA

Naibu   Waziri   wa Mambo  ya   Ndani   ya   Nchi,   Mhandisi   Hamad   Masauni,akiwaongoza   Wajumbe   wa   Kamati   ya   Ulinzi   na   Usalama   ya   Wilaya   yaKilindi   kuingia   Kituo   cha   Polisi   cha   Songe, ikiwa   ni ziara   ya   kikazi   yaNaibu   Waziri   kukagua   shughuli   za   ulinzi   na   usalama   wilayani   Kilindimkoani Tanga .Picha  na  Wizara  ya Mambo  ya  Ndani  ya  Nchi 
Naibu   Waziri   wa Mambo   ya   Ndani   ya   Nchi,   Mhandisi   Hamad   Masauni,akizungumza katika kikao cha ndani kilichohusisha   Wajumbe   wa   Kamati   yaUlinzi  na  Usalama  ya  Wilaya  ya Kilindi  ikiwa  ni ziara  ya  kikazi  ya  NaibuWaziri   kukagua   shughuli   za   ulinzi   na   usalama   wilayani   Kilindi   mkoaniTanga  .  Kushoto ni  Mkuu wa Wilaya  ya  Kilindi,  Sauda  Mtondoo  na  Kulia  niKatibu  Tawala  wa  Wilaya  hiyo,  Warda  Abeid. Picha na Wizara ya Mambo yaNdani  ya  Nchi
Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Sauda  Mtondoo   akizungumza  katika  kikao  chandani kilichohusisha  Wajumbe  wa  Kamati  ya  Ulinzi  na  Usalama  ya  Wilayaya Kilindi  ikiwa  ni ziara  ya  kikazi  ya  Naibu  Waziri  wa  Mambo ya Ndani yaNchi,   Mhandisi   Hamad   Masauni   (katikati)   kukagua     shughuli     za     ulinzi     nausalama  wilayani  Kilindi  mkoani Tanga . Kulia ni  Katibu  Tawala  wa  Wilayahiyo, Warda  Abeid. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani  ya  Nchi
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi , EdwardBukombe,  akizungumza  katika   kikao   cha  ndani  kilichohusisha    Wajumbe    waKamati  ya  Ulinzi  na  Usalama  ya  Wilaya  ya Kilindi  ikiwa  ni ziara  ya  kikaziya   Naibu   Waziri   wa   Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani, ) kukagua   shughuli   za  ulinzi   na  usalama  wilayani   Kilindimkoani Tanga . Picha  na  Wizara  ya Mambo  ya  Ndani  ya  Nchi


Serikali imedhamiria kujenga Vituo vya Polisi 65 katika wilaya mbalimbali nchiniikiwa ni juhudi za kukabiliana   na uchakavu na upungufu wa vituo vya polisinchini.

Hayo   yamesemwa   na   Naibu   Waziri   wa   Mambo   ya   Ndani   ya   Nchi,   MhandisiHamad Masauni   baada ya kutembelea na   kukagua  Kituo cha Polisi cha   Songeambacho ndio kituo kikuu katika Wilaya ya Kilindi mkoani Tanga

Alisema Serikali inatambua changamoto za vituo vya polisi ikiwemo uchakavu,udogo   wa   majengo   katika   vituo   mbalimbali   nchini   na   iko   katika   mpango   wakujenga vituo vya polisi 65 ili kuwepo na ulinzi thabiti wa raia na mali zao.

“Serikali   inatambua   changamoto   ya   vituo  vya   polisi  hasa   katika  wilaya   mpyanchini, ikiwepo uchakavu wa majengo, kwahiyo uko mkakati maalumu wa kujengavituo vya polisi 65 nchi nzima ili kuweza kukabiliana na matukio ya kiuhalifu,lengo la serikali ni kuhakikisha raia wake na mali zao zinakua salama na matukioya kiuhalifu yanapungua na kutoweka kabisa,” alisema Masauni

Alisema Serikali pia inakaribisha nguvu za wananchi na wadau mbalimbali ambaowako tayari kusaidia ujenzi wa vituo vya polisi huku akipongeza baadhi ya maeneonchini  ambako   vituo  vya  polisi  vimejengwa   kwa  ushirikiano  wa  michango   yawananchi na serikali.

Awali akitoa taarifa ya Ulinzi na Usalama  ya Wilaya ya Kilindi, Mkuu wa Wilayaya  Kilindi   na  Mwenyekiti   wa  Kamati   ya   Ulinzi   na  Usalama,   Sauda  Mtondooalisema hali ya uhalifu kuanzia kipindi cha Januari hadi Oktoba 2018 ilikua yawastani huku kukiripotiwa upungufu wa makosa kwa asilimia 9.8 kati ya mwaka2018 na 2017.

“Kwa mujibu wa takwimu za uhalifu kulikuwa na jumla ya makosa makubwa yajinai 163 ndani ya mwaka huu yaliyoripotiwa kwa kulinganisha na makosa 179yaliyoripotiwa ndani ya mwaka 2017, ukiwepo upungufu wa makosa 16 katikavipindi hivyo viwili,” alisema Sauda

Akizungumza   wakati   wa   ziara   hiyo,   Mbunge   wa   Kilindi,   Omari   Kibuaalimshukuru  Naibu Waziri kwa kufika jimboni hapo kujionea hali halisi ya kituohicho kikuu cha wilaya  baada  ya  kumuomba  kufanya  hivyo wakati wa kikaocha bunge kilichomalizika hivi karibuni

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.