ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 15, 2018

LIVERPOOL WAWEKA MEZANI KITITA KUMNASA DEMBELE.



Klabu ya Liverpool inajianda kuweka mezani kitita cha pauni milioni 85 kwaajili ya kumsajili nyota wa Barcelona, Ousmane Dembele dirisha lijalo la mwezi wa Januari.

Mfaransa huyo ameshindwa kabisa kuendana na mfumo ndani ya Nou Camp hali inayopelekea kushindwa kuwa na nafasi ya uhakika ya kucheza tangu aliposajiliwa kutoka Borussia Dortmund  kwa dau nono lililoweka rekodi ya dunia ya pauni milioni 135.

Kwa mujibu wa ripoti kutoka ndani ya Liverpool meneja wa timu hiyo Jurgen Klopp yupo tayari kuweka kitita cha fedha kwaajili ya kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21.

Klopp anaamini kuwa usajili wa nyota huyo utasaidia kuongeza nguvu ndani ya kikosi chake kwenye mbio za kuwania ubingwa.

Hata hivyo kwa sasa Majogoo hao wa Uingereza wapo vizuri hasa kutokana na uwepo wa Mohamed Salah, Sadio Mane, Roberto Firmino na Daniel Sturridge.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.