ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 22, 2018

FUNDI ALIYEOKOLEWA HII HAPA SABABU YAKE KUBAKI HAI



GSENGOtV

Baada ya mamia kunasuliwa wakiwa tayari wameaga dunia, imekuwa faraja kwa maelfu ya watu waliofurika kwa wingi hii leo katika eneo la hospitali ya Bwisya, Ukara, ambao walijikuta wakilipuka kwa furaha, baada ya Fundi mkuu wa meli iliyopinduka na kuzamisha mamia ya watu, Alphonce Cherehani kupatikana akiwa hai na kuokolewa.

Imeelezwa kuwa Mhandisi Alphonce Charahani aliyeokolewa akiwa hai kwenye ajali ya MV Nyerere leo, alikuwa amejifungia kwenye chumba maalum na kujipaka oili mwilini ili maji yasipite kwenye vinyweleo vyake kuingia mwilini. (ZAIDI VIDEO)
Cherehani ameongeza idadi ya waliosalimika kuwa 41.

Idadi ya watu waliopoteza maisha katika ajali ya Kivuko cha MV Nyerere sasa imefikia 218.

Waliotambulika ni 172 na ambao hawajatambuliwa na ndugu zao ni 46

Kwamujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella, amesema kwa sasa taratibu mbalimbali zinaendelea kufanyika ikiwa ni pamoja na jitihada za kukinyanyua kivuko hicho kazi ambayo itafanywa na timu ya waokoaji iliyonjiani kuingia eneo la ajali.

“Kesho kuanzia saa 2 asubuhi kamati itafanya maziko ya miili 47”, amesema Mongella.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.