ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 2, 2018

MASAUNI ZIARANI WILAYANI BUNDA KUKAGUA NA KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA ASKARI POLISI

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani  ya  Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akikagua mojaya makazi ya askari polisi   katika   kijiji cha Makongoro B,   kilichopo wilayani Bundawakati wa ziara ya kikazi ya kukagua na kushughulikia changamoto za makazi ya askaripolisi   ambapo jumla ya nyumba mia nne   za askari polisi zinatarajiwa kujengwa nchinzima.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi


Naibu  Waziri wa   Mambo   ya Ndani    ya     Nchi,   Mhandisi   Hamad   Masauni,   akisomamaelezo ya mmoja ya mtuhumiwa  aliyemkuta katika chumba cha mahabusu katika Kituocha   Polisi   Bunda   wakati   wa   ziara   ya   kikazi   ya   kupitia   shughuli   za   utekelezaji   wamashtaka ya mahabusu walioko katika vituo vya polisi nchini.Wapili kulia ni Mkuu waWilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili na wengine ni viongozi waandamizi wa kamati yaUlinzi na Usalama wilayani  Bunda.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Afisa Mnadhimu wa Polisi mkoa wa Mara, Mrakibu Mwandamizi ,Jeremiah Shila  akitoamaelezo ya mwenendo wa mashtaka ya watuhumiwa walioko katika Kituo cha PolisiBunda   kwa  Naibu   Waziri   wa   Mambo   ya   Ndani   ya   Nchi,   Mhandisi   HamadMasauni(wapili kulia) na   Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili(watatu kulia),wakati   wa   ziara   ya   naibu   waziri     kupitia   shughuli   za   utekelezaji   wa   mashtaka   yamahabusu walioko katika vituo vya polisi nchini. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndaniya Nchi


Naibu   Waziri   wa   Mambo   ya     Ndani     ya     Nchi,   Mhandisi   Hamad   Masauni   (watatukushoto),   akifuatilia   wakati   mpelelezi   akifunua   jalada   la   mmoja   wa     mahabusualiyemkuta katika chumba cha mahabusu katika Kituo cha Polisi Bunda wakati wa ziaraya kikazi ya kupitia shughuli za utekelezaji wa mashtaka ya mahabusu walioko katikavituo vya polisi nchini.Wapili kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili nawengine   ni   viongozi   waandamizi   wa   kamati   ya   Ulinzi   na   Usalama   wilayaniBunda. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Serikali Kujenga Nyumba 400 za Askari  Polisi Na Mwandishi WetuSerikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni kumi kwa ajili ya ujenzi wa nyumba zaaskari polisi kote nchini, ikiwa ni kukabiliana na changamoto ya makaazi ya askarina uchakavu wa vituo vya polisi ili kuwawezesha askari hao kutekeleza majukumuyao kwa ufanisi. 

Hayo yamesemwa     na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, MhandisiHamad  Masauni alipotembelea   kijiji   cha  Makongoro   wilaya  ya   Bunda  mkoaniMara   kuona   changamoto   wanazokutana   nazo   askari   polisi   katika   kutekelezamajukumu yao ya ulinzi na usalama.

Alisema wizara iko katika mpango maalumu wa kuboresha makazi ya askari polisinchini huku akitoa  wito na nafasi kwa  wadau wa maendeleo pia  kujitokeza nakuunga  mkono  juhudi  za  Rais   Dk.John  Magufuli kuboresha makazi  ya  askaripolisi “Katika kukabiliana na changamoto ya askari nchi nzima tayari tushaanza kujengamakazi ya askari wetu tukianza na nyumba za polisi Kusini Pemba na tutaendeleana ujenzi huo wa nyumba 400 katika mikoa mingine nchini na kutokana na haliniliyoiona   hapa   Bunda   basi   tutatoa   kipaumbele   hapa”Alisema   Naibu   Waziri Masauni Akizungumza wakati wa ziara hiyo

Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili, ametoa rai kwa wananchi kuhakikisha wanashirikiana na serikali katika ujenzi wamakazi ya askari polisi wilayani humo huku Mwenyekiti wa Kijiji hicho Mussa Masilu akiongeza   kuwa nyumba hizo ni chakavu na zinashusha hadhi ya Askari Polisi.

Hadi sasa serikali imeshaanza taratibu za awali ikiwemo tathmini ya ujenzi wanyumba hizo mia nne za askari polisi nchini ambapo mikoa mbalimbali itanufaikana  ujenzi huo utakaotekelezwa kwa awamu tofauti ukienda sambamba na ujenzina ukarabati wa vituo vya polisi. ……………………………......................MWISHO………………………………………..

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.