ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 20, 2018

SAUTI - CHADEMA NJOMBE WALAANI VIKALI WAGOMBEA WAO KUKATALIWA NA WASIMAMIZI CHANZO WATAJWA KUWA SI RAIA



GSENGOtV
NJOMBE

Chama cha demokrasia na maendeleo Chadema mkoani Njombe kimelani Vikali Kitendo cha wasimamizi wakuu wa Uchaguzi katika halmashauri ya Wilaya ya Makete na Wanging'ombe kwa kuyaondoa Maajina ya mwagombea wake wawili wa udiwani katika Kata ya Isapulano na Itulahumba kwa madai ya kwamba wamekosa sifa za kuwania nafasi hiyo.

Msmamizi mkuu wa uchaguzi wilayani Makete ambae pia ni mkurugenzi wa halmashauri hiyo Fransis Namaumbo Anatajwa kumuondoa mtia nia wa Chadema katika kata ya Isapulano ndugu Dadiso Tweve kwa madai ya kwamba sio mkazi huku mkurugenzi wa halmashauri ya Wanging'ombe Amina Kiwanuka Akimuondolea Sifa ya kugombea Mgombea wa Kata ta Itulahumba Mgute Yohane kwa madai ya kutilia shaka mihuli iliyopigwa kwenye fomu yake.

TAARIFA KUTOKA NJOMBE INASOMWA NA AMIRI KILAGALILA


Kata ya Isapulano ya wilayani Makete inalazimika kurudia uchaguzi Augost 12 baada ya diwani wake kujiuzuru na kujiunga na chama cha mapinduzi huku katika kata ya Itulahumba ya wilayani Wanging'ombe ikirejewa baada ya diwani wake kufariki dunia.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.