ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, June 7, 2018

TANZIA:- MSANII WA BONGO FLEVA SAM WA UKWELI HATUNAYE.

Enzi za uhai wake msanii Sam wa Ukweli.

GSENGOtV
Msanii wa Bongo Fleva, Sam wa Ukweli amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Palestina, Sinza jijini Dar baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Chanzo cha kifo chake kimelelezwa na Producer wake Steve kuwa “Sam alianza kuzidiwa toka J’mosi, tulipomuuliza anaumwa nini alisema ukimwi lakini sio ukimwi wa kawaida bali wa kulogwa”

Mwili wa marehemu umepelekwa katika hospitali ya Mwananyamala kuhifadhiwa.


Sam aliwahi Ku-Hit na ngoma zake kama vile Sina Raha, Milele, Kisiki, Ameolewa aliyowashirikisha wakali Z-Anto na Rich Mavoko na nyingine nyingi ambazo licha ya kukubalika majumbani kwa wakubwa na watoto pia alitumika sana katika majukwaa ya kampeni mbalimbali za kijamii, huduma za afya na vilevile majukwaa ya siasa hasa uchaguzi mkuu uliopita ulioiweka madarakani Serikali ya Rais John Pombe Magufuli, ambapo yeye alikisimamia barabara chama hicho kwenye kampeni zake kama picha mbalimbali zinavyoonekana hapa chini.




Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.