ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 24, 2018

ZIARA YA KATIBU MKUU, MAALIM SEIF SHARIF HAMAD KATIKA JIJI LA MWANZA:




THE CIVIC UNITED FRONT
(CUF –Chama Cha Wananchi)
THE DIRECTORATE OF INFORMATION, PUBLICITY AND PUBLIC RELATION
P.O. BOX 3637 Zanzibar, Tanzania
TAARIFA KWA UMMA NA VYOMBO VYA HABARI
ZIARA YA KATIBU MKUU, MAALIM SEIF SHARIF HAMAD KATIKA JIJI LA MWANZA:
Leo Tarehe 23/5/2018 saa 10 Jioni Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad atawasili Jijini Mwanza na kupokelewa na Wanachama na Viongozi wa CUF wa ngazi mbalimbali za Chama. Katibu Mkuu ataongozana katika msafara huo na Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui na Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma Mhe. Mbarala Maharagande, atakuwa Mwanza kwa ziara ya siku Tatu baada ya kupata mualiko kutoka kwa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UNION OF TANZANIA PRES CLUB-UTPC) yenye makao yake Makuu Mkoani Mwanza. UTPC- kwa sasa ina klabu wanachama (Press Clubs) 28 toka Tanzania Bara na Visiwani.
UTPC kwa kushirikiana na vyombo vya Habari inaendesha kipindi cha TUJADILIANE kinachowakutanisha waandishi wa Habari kutoka katika redio zote zilizopo Mkoani Mwanza, TV pamoja na magazeti na imekuwa ikiwaalika wageni kutoka Serikalini, Asasi za kiraia, na watu mashuhuri wakiwemo wanasiasa kutoka hapa nchini. Pamoja na shughuli zingine kesho Tarehe 24/5/2018 kuanzia saa 5 kamili asubuhi katika ukumbi wa hotel ya JB BELMOUNT Jijini Mwanza atashiriki katika kipindi maalumu cha TUJADILIANE. Katika kipindi hicho Maalim Seif atapata fursa kuelezea masuala mbalimbali ya kisiasa, kiuchumi na jamii kwa ujumla na pia atapata fursa ya kuelezea DIRA YA CUF, MWELEKEO WA CUF, MAFANIKIO YA CUF, CHANGAMOTO ZINAZOIKABILI CUF NA NAMNA YA UTATUZI WAKE.
Katibu Mkuu, Maalim Seif atakutanishwa na waandishi wa habari wa Jijini Mwanza na mahojiano ya kipindi hicho yatarushwa MUBASHARA “LIVE” kupitia mitandao ya kijamii hususani Facebook, na pia yatasikika kupitia Radio SAUT, RFA, Kiss FM, Afya Radio, Metro FM, Radio Sengerema, HSC, Living water, Ukombozi FC, Iqra FM, Kwa Neema Radio za Jijini Mwanza na Safari FM ya Mkoani Mtwara. Pia kupitia Facebook Account ya Julius Mtatiro na links zingine mbalimbali. Na baadae katika vipindi vya Television. Pamoja na kuwa uso kwa uso na jopo la waandishi wa habari Jijini Mwanza, mahojiano hayo yatakayoongozwa na Ndugu Dotto Emmanuel Bulendu.
Tunapenda kuchukua fursa hii kuwajulisha rasmi Programu hiyo kwa ufuatiliaji na kama kuna masuala ambayo unahitaji Maalim Seif aulizwe usisite kututumia na au kumtumia mratibu wa kipindi hicho Dotto Bulendu kupitia akaunti yake ya Facebook.
HAKI SAWA KWA WOTE
………………………
SALIM BIMANI
MKURUGENZI WA HABARI, UENEZI NA MAHUSIANO NA UMMA
MAWASILIANO: 0777 414 112/ 0752 325 227
Imetolewa leo Tarehe 23/5/2018

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.