ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 27, 2018

BABU SEYA NA MWANAE KUANGUSHA BURUDANI YA KUFA MTU KWA WAKAZI WA MWANZA


KWA mara ya kwanza wakazi wa Mwanza na mikoa jirani wanakwenda kushuhudia burudani waliyoikosa kwa muda mrefu katika tasnia ya muziki wa bendi pale ambapo wakali wa siku nyingi kwenye muziki huo Nguza Viking na mwanae Papii Kocha watakapo shuka jijini humo na kutoa burudani ya muziki live.

Papii kocha aliyetamba na kazi zake kama Salima, Fanta, Moyo, na Seya ngoma aliyoimba na baba yake Nguza Viking kwa hivi sasa anatamba na mkwaju wake mpya unaoitwa 'Waambie'.

Daaah huyu jamaa niliwahi kusema akirudi kuimba Tena Dunia itasimama.

Yasome mashairi yake hapa.

Verse 1.

Dunia inazama, naangalia, 
Sina cha kufanya,moyoni naumia.
Mawazo yangu oh, naangamia
Uko wapi Mungu wangu we,hunioni nalia

*Kumbe ulikua unanisikia , unaniangalia.....weweeee
Likapotea,tumaini langu ila imani ikaingiaa....×2

Chorus

Waambie, uliniona,nilipokuomba uliskia,na ukaitika.
Mungu wambie,uliposema uwaja, wala hukukosea njia, na ulifika.
Mungu wambieee, niwewew tuuu, niwewee tuuu, wuwuwu.
Mungu wambie eeh, niwewe tuu uliesababisha leo imefika.

Verse 2.
Wambie, kila siku ni zawadi, hakuna heshima inayozidi uhai.
Ni Nineema na Rehema, wawe ha hekima unazitimiza ahadi,
Ooh ooh wambie, hawapaswi kukata tamaa, sababu daima haupo mbali.
Ukipotea mwanga, gizani ndo nyota hunga'aa mwanga mkali.

Wambie, 
Wasiache tumaini ndo imaniiii iii
Wasiache kukuamini ndo amanii ii iii

Chorus

Waambie, uliniona,nilipokuomba uliskia,na ukaitika.
Mungu wambie,uliposema uwaja, wala hukukosea njia, na ulifika.
Mungu wambieee, niwewew tuuu, niwewee tuuu, wuwuwu.
Mungu wambie eeh, niwewe tuu uliesababisha leo imefika. ×2



Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.