ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 5, 2018

SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR YAZINDUA UGAWAJI ENDELEVU WA VYANDARUA VYENYE DAWA YA MUDA MREFU.

Na Ferdinand Shayo,Arusha .
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Charles Mkumbo amekanusha vikali maonyesho ya Jeshi la polisi yanayoambatana na mazoezi  ya jeshi hilo yanayoendelea  katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid vilivyoko jijini Arusha  kuhusishwa na maandalizi ya kukabiliana na maandamano yanayohamasishwa kwenye mitandao na kudaiwa  kufanyika april 26.

Mkumbo amesema kuwa  maonyesho hayo ni ya kawaida na jeshi hilo limekua likijiweka imara kwa ajili ya kulinda raia na  mali zao na taifa kwa ujumla na si maandamano ambayo ni ya kusadikika .

Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake amesema kuwa maonyesho hayo yatafanyika April 7 baada ya kuzindua nyumba za kuishi za jeshi la polisi zitakazozinduliwa na Raisi John Pombe Magufuli.

Aidha amewakaribisha wananchi wa Jiji la Arusha kujitokeza kwa wingi kuona maonyesho ya kazi za jeshi hilo lenye jukumu la kulinda raia na mali zao.

Kamanda amesema kuwa licha ya uzinduzi wa nyumba hizo wanatarajia kuzindua kituo cha utalii na diplomasia ambacho kitasaidia shughuli za utali na kuchochea ari ya watalii kutembelea mkoa wa Arusha wenye vivutio vingi.

Alisema kuwa mpaka sasa maandalizi yako vizuri ya kumpokea Raisi na wanatarajia hakutakua na msongamano wa magari kwani shughuli za kila siku zitaendelea kama kawaida.

Hata hivyo ametoa onyo kali kwa wanaoharibu miundombinu ya barabara ikiwemo alama za barabarani na kusababisha adha kwa watumiaji wa barabara kwani jeshi hilo halitawavumilia  na hatua kali zitachukuliwa .

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.