ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, February 15, 2018

SAA 48 ZILIZOMNG'OA ZUMA MADARAKANI.

President of South Africa Jacob Zuma addresses the nation at the Union Buildings in Pretoria on February 14, 2018.
Jacob Zuma, ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya Urais. REUTERS
KWA HISANI YA BBC SWAHILI.
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amejiuzulu baada ya shinikizo nyingi kutoka kwa chama chake. Hatimaye Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ajiuzulu
Kapitia hotuba yake iliyopeperushwa kwa njia ya televisheni alisema anajiuzulu mara moja lakini akaongeza kuwa hakubaliani na uamuzi wa chama cha ANC.
Chama cha ANC kilikuwa kimemuambia aondoke madarakani au akabiliwe na kura ya kutokuwa na imani naye bungeni.
Zuma mwenye umri wa miaka 75 amekuwa akikabiliwa na shinikizo za kumtakja ampe nafasi mamamu wake Cyril Ramaphosa, ambaye ndiye sasa kiongozi mpya wa chama.
Bw Zuma ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 2009, amekumbwa na shutuma nyingi za ufisadi.
Mapema Jumatano, polisi walivamia nyumba ya familia tajiri ya Gupta ambayo Zuma ana uhusiano wa karibu nayo.

Zuma alijiuzulu kwa njia gani?

Alianza hotuba kwa kucheka na kufanya mzaha na waandishi wa hahari.
Baada ya kuwashukuru wale ambao amefanya kazi nao kwa miaka kadhaa, Bw Zuma alisena kuwa ghasia na migawanyiko ndani ya ANC imesabisha ajiuzulu.
"Hakuna maisha itapotea kwa sababu yangu wala ANC haiwezi kugawanyika kwa sababu yangu. Kwa hivyo nimefikia uamuzi wa kujiuzulu kama rais wa nchi mara moja," alisema
"Licha ya kutokubaliana na uamuzi wa chama changu, siku zote nimekuwa mwanachama mwenye nidhamu wa ANC.
"Ninapoondoka, niataendelea kuwatumikia watu wa Afrika Kusini sawa na ANC, chama ambacho nimekitumikia maisha yangu yote."



Jacob Zuma ni Rais wa aina yake na mwenye utata kuwahi kutokea Afrika Kusini

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.