ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 4, 2018

BAADA YA BENKI KUU KUZIFUNGA BAADHI YA BENKI NCHINI WANANCHI WENYE FEDHA ZAO WALIOKUWA WAKIHITAJI KULIPA ADA ZA WATOTO WAO WAHAHA

NJOMBE
Baadhi ya wananchi na wateja wa benk ya wananchi Njombe NJOCOBA wameanza kukutana na ugumu wanapohitaji kuzipata huduma za kibenk mara baada ya benk hiyo kutangazwa kufungwa na benk kuu ya Taifa.

Na.amiri kilagalila
Wakizungumza hii leo mara baada ya kufika katika ofisi za benk hiyo ili kupata huduma na kukuta imefungwa,wamesema kuwa hali kwa sasa itakuwa ngumu kwao kutokana na maandalizi ya watoto kwenda shule huku fedha yao ikiwa imehifadhiwa katika benk hiyo.
Insert…………………………….wananchi
Mara baada ya kuzungumza na wateja nje ya benki hiyo nimehitaji kupata ufafanuzi kwa wahusika juu ya swala hilo ambalo limeanza kuonekana ni changamoto kwa baadhi ya wateja ambapo nimekutana na askari wa jeshi la polisi pamoja na mmoja wa watumishi katika benki hiyo na kusema kuwa kwa sasa swala hilo lipo mikononi mwa benki ya Taifa.
Insert…………………………………….polisi na mtumishi
Aidha mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Njombe ERDWIN MWANZINGA ambapo ndipo inapatikana benk alikuwa karibu na mazingira ya benki hiyo hii leo na kusema kuwa huenda benk kuu imefikia uamuzi wa kuifunga benk ya NJOCOBA kutokana na kushindwa kutoa huduma na kuwaomba wananchi kuwa watulivu kutokana na fedha walizozihifadhi.
Insert…………………..mwanzinga
Hata hivyo kwa kipindi kifupi kilichopita Benki ya Wananchi Njocoba imekuwa ikilalamikiwa kwa kushindwa kutoa huduma za kifedha kwa wakati hali iliyowalazimu wateja kuwa na shaka kufilisika kwake mapaka hii leo kuwa miongoni mwa benk zilizofungiwa, aidha benki nyingine zilizofungiwa na kufutiwa leseni zao na benki ya taifa hii leo ni pamoja na COVEANAT Bank, Efata Bank Limited, Kagera Farmers Cooperative Bank Limited na Meru Community Bank Limited.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.