ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, October 19, 2017

USAID WARIDHISHWA NA KASI YA MKOA WA MWANZA NA MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA

 Wakiwa na nyuso za furaha wanafunzi wa shule ya msingi Sese ni muda wa kutawanyika kuelekea majumbani kwao baada ya masomo, vilevile hapa ni baada ya kupokea msaada wa vyandarua walivyogawiwa bure kutoka USAID.
 Wadau kutoka USAID walipata fursa pia kutembelea Zahanati ya Sese.
 Watoto hawa wanatambua umuhimu wa vyandarua.
Kufanikiwa kwa juhudi za kutokomeza ugonjwa wa malaria kutaufanya ulimwengu kuwa mahala pazuri na salama pa kuishi kwa kizazi na vizazi vijavyo na kuwawezesha mamilioni ya watu kufikia malengo yao kimaisha.
Binagi Media Group
Mapambano dhidi ya ugongwa hatari wa Malaria yameendelea kuonyesha mafanikio mkoani Mwanza, baada ya vifo vitokanavyo na ugonjwa huo kupungua kutoka asilimia 19.01 mwaka 2011/12 hadi asilimia 15.1 mwaka 2015/16.


Hiyo ni kutokana na juhudi za serikali kupambana na ugonjwa huo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo shirika la misaada la watu wa Marekani USAID ambalo limeendelea kusaidia vyandarua vyenye kinga kwa ajili ya mapambano dhidi ya malaria.

Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza, Dkt.Leonard Subi aliyasema hayo jana wakati wa zoezi la kugawa vyandarua bure katika shule ya Msingi Senge iliyopo Kata ya Bujashi wilayani Magu ambalo lilishuhudiwa pia na ujumbe kutoka USAID Marekani.

Alisema mbali na kuua vimelea vya Malaria kwa kutumia viuatilifu, pia serikali inagawa vyandarua bure katika shule za msingi, vituo vya afya, zahanati pamoja na hospitali ili kuongeza kasi ya mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

Monica Ngalula pamoja na Marco Yusuph ni baadhi ya wanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya msingi Sese, walishukuru kwa kugawiwa vyandarua hivyo na kwamba vitawasaidia wasing’atwe na mbu wa Malaria wakiwa wamelala nyumbani kama ilivyokuwa hapo awali.

Mkurugenzi wa Mawasiliano kutoka USAID, Chriss Thomas alifurahishwa na juhudi za Tanzania kupambana na ugonjwa wa Malaria na kuahidi ushirikiano zaidi wa kusaidia mapambano hayo ili kuokoa maisha ya watu hususani akina mama wajawazito pamoja na watoto ambao wamekuwa kwenye hatari ya kupoteza maisha kutokana na ugonjwa huo.
Mganga Mkuu mkoani Mwanza, Dkt.Leonard Subi
Mkurugenzi wa Mawasiliano kutoka USAID, Chriss Thomas akizungumza na wanahabari
Ujumbe kutoka USAID Marekani ukiwa shule ya msingi Sese wilayani Magu kushuhudia zoezi la ugawaji vyandarua
Mwanafunzi wa shule ya msingi Sese akipokea chandarua kutoka USAID
Mwanafunzi wa shule ya msingi Sese akipokea chandarua kutoka USAID
Ugeni kutoka USAID Marekani
Shule ya msingi Sese wilayani Magu ni miongoni mwa shule za msingi 941 ambazo wanafunzi wake wananufaika na zoezi la ugawaji vyandarua bure mkoani Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.