ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, October 20, 2017

NAPE AMFINYA LISSU "TULIA KWANZA UPONE KABISA KABLA HUJASEMA MENGI"



Mbunge wa jimbo la Mtama kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Nape Nnauye amefunguka na kusema amefurahi kumuona Tundu Lissu akiwa katika furaha na tabasamu na kumuomba kwa sasa asiseme lolote mpaka pale atakapona kabisaa.
Nape Nnauye amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter na kusema tabasamu la Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akiwa kwenye hospitali jijini Nairobi linatoa matumaini makubwa.
"Mjomba tunamshukuru Mungu kwa tabasamu hili la matumaini!Nakuombea afya iimarike kabla hujasema mengi! Tulia mjomba upone kabisa kwanza" alisema Nape Nnauye

Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu alishambuliwa na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa mjini Dodoma nyumbani kwake na baadaye alipelekwa jijini Nairobi kwa matibabu zaidi ambapo mpka sasa anapatiwa matibabu huko.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.