ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, October 3, 2017

MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BIMA NCHINI TIRA YATOA MAFUNZO KWA ASKARI WA KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI MKOANI PWANI KUPAMBANA NA BIMAFEKI

  Askari wa kikosi cha usalama barabarani Mkoa wa Pwani Laitiness Kimaro akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani mara baada ya kumaliza mafunzo yanayohusiana na mfumo mpya wa kuwabaini baadhi ya madereva na wamiliki ambao wamekuwa wakitumia stika za bima feki kinyume cha sheria na taratibu.(PICHA NA VICTOR MASANGU)

 Mmoja wa askari wa kikosi cha Usalama barabarani Mkoa wa Pwani  Khalid Mohamed akifafanua jambo mara baada ya kumaliza mafunzo ya jinsi ya  mfumo mpya unaotumika katika kuwabaini madereba hao wanaotumia bima feki.

 Baadhi ya askari wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Pwani wakiwa wanaendelea na zoezi la kufanya ukaguzi kwa baadhi ya magari ambayo yanatumia stika za bima bandia.

 Kaimu kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani Blasilusi Chatanda akizungumza na baadhi ya waandishi wa habari nje ya ukumbi wa maisha plus ambapo yamefanyika mafunzo kwa askari wa usalama barabarani juu ya mfumo mpya wa kukagua magari ili kuweza kubaini wanaotumia bima feki kinyume na taratibu.(PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU)

KATIKA kukabiliana na kupambana na  wimbi la wizi linalofanywa na  baadhi ya wamiliki wa  magari na pikipiki  kuamua kutumia stika za bima bandia hatimaye  Mamlaka ya usimamizi wa shughuli za  bima  nchini (TIRA) imeamua kutoa mafunzo kwa askari wa kikosi cha usalamaa barabarani Mkoa wa Pwani kwa lengo la kuweza

Akizungumza katika mafunzo hayo ambayo yamewashilikisha maafisa wa polisi pamoja na askari wa kikosi cha usalama barabarani Kamishina mkuu wa (TIRA) nchini Baghayo Sakwele lengo la amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kwa ajili ya kuweza kuwafundisha askari wa usalama barabarani mfumo mpya ambao utaweza kuwasaidia kutambua na kuhakiki stika za bima ambazo ni bandia na zinatumika kinyume kabisa na sheria na taratibu.

Kamishina  huyo alibainisha kuwa kwa sasa wameamua kushirikiana na jeshi la Polisi ili kuweza kufanya msako wa kuweza kuwabaini wamiliki wa vyombo vya moto kutumia bima feki kitu ambacho kinachangia kwa kiasi kikubwa kupoteza kwa pato la Taifa kutokana na  vitendo vya wizi ambavyo vinafanyika, na kuongeza kuwa changamoto iliyopo ni wamiliki wengine  wanafanya ujanja wa kutumia bima moja zaidi ya magari matano.

“Sisi kama TIRA ambao ndio wenye mamlaka ya utoaji wa stika za bima katika vyombo vya magari, tumeamua kushirikiana bega kwa began a jeshi la polisi Mkoa wa Pwani ili kuweza kuhakikisha kuwa wale baaadhi ya wamiliki waliokuwa na tabia ya kutumia magari yao au pikipiki kwa kutumia bima bandia tunawakamata na kuwachukulia hatua kali za kisheria na katika hili hatuwezi kuwavulimilia hata kidogo,”alisema Kamishina Sakwele.

Kwa upande wake Kaimu kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani Blasilusi Chatanda alisema  kuwa atalivalia njuga suala hilo la kufanya msako mkali ili kuweza kubaini mtandao unaojihusiha na kutengeneza bima feki ili kuweza  kuwathibiti wale wote ambao walikuwa wanatumia bima bandia kuwachukulia hatua kali za kisheria ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.

“Kama jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na wenzetu wa  Tira kwa kweli tutashirikiana nao kwa hali na mali na kwa kuwa wameshatupatia mafunzo kuhusiana na mambo mbali mbali ikiwemo kuwepo kwa wimbi la madereva na wamiliki wa vyombo vya moto kuwa na tabia ya kutuia stika za bima feki tunawakamata na kuwachukulia hatua kali za kisheria kwa hivyo vaskari wetu nina imani walilifanikisha suala hilo,”alisema Kamanda.

Nao baadhi ya askari wa kikosi cha usalama barabarani Mkoa wa Pwani ambao wameshiriki  katika mafunzo hayo akiwemo George Peter, Laitiness Kimaro pamoja na Khalid Mohamed  wamesema kuwa yatawasaidia katika kutekeleza majukumu yao ipasavyo katika masuala mbali mbali ya kuwaelimisha  madereva wa magari na pikipiki kuhusiana na bima feki na iliyo halali.

Walisema kuwa wana imani kuwa baada ya kujifunza  mafunzo hayo wataweza kufanya kazi zao za barabarani kwa ufanisi mkubwa zaidi na kuhakikisha wanatoa elimu ya kutosha kwa madereva wote wa vyote vya moto ikiwemo magari pamoja na pikipiki kuhusiana na matumizi halali ya ukataji wa bima zao pamoja na madhara ya kukata bima amabzo ni feki.

“Kwa kweli sisi kama askari wa kikosi cha usalama barabarani katika Mkoa wa Pwani tumefarijika sana kuuaptiwa mafunzo haya na wenzuetu wa mamlaka ya husika, hivyo na sisi tutahakikisha elimu hii inakuwa ni chachu na mkombozi mkubwa katika utekelezaji wa majukumu yetu ya kila siku pindi tuapokuwa barabarani hivyo ni jambo ambalo kwa kweli ni faida kwetu,”walisema askari hao.

ASKARI hao wa kikosi cha usalama barabarani Mkoa wa Pwani mara baada ya kupatiwa mafunzo hayo walikwenda kufanya ukaguzi wa magari  barabarani kwa njia ya vitendo zaidi ambapo  katika zoezi hilo walisewe kufanikiwa kukamata baadhi ya  magari na kuyapiga faini  ambayo yamekuwa bado yakiendelea  kutumia  bima feki kinyume na sheria za nchi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.