ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 10, 2017

ANNA MGHWIRA AMNG'OA KIONGOZI ACT- WAZALENDO

Ikiwa ni Siku chache baada ya Mwenyekiti wa Chama cha Act-Wazalendo Anna Mghwira kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkao wa Kilimanjaro leo ameibuka Katibu wa chama hicho Mkoa wa Mbeya  Bahati Longopa na kutangaza kujiuzuluzu nafasi hiyo kwa alichodai kutoridhia uteuzi huo.

Longopa amesema  kuendelea kuwa kiongozi wa chama kutampa wakati mgumu kuhamasisha wanachama wapya katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2020.

Amesema kuwa kwa hiari yake ameacha nafasi hiyo ndani ya chama kutokana na kitendo cha viongozi wa juu wa Chama hicho kuingia ndani ya Serikali iliyopo madarakani ambayo ni ya chama pinzania kwao wao viongozi wa chini hawataweza kuwashawishi wanachama wapya kujiunga na chama hicho

Kuhusu kujiunga na chama  kingine cha siasa amesema kwa sasa ni mapema mno kuzungumzia hilo kwani   ataendelea kukaa pembeni na kutojihususisha kwenye mambo ya siasa  huku akitafakari nini cha kufanya.

Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo,   Wilaya ya Mbeya, Ally Mbika alisema wamepata taarifa  za chini chini, lakini kama chama bado hawajakabidhiwa barua yoyote kutoka kwa kada huyo kutamka kujiuzulu rasmi.


Amesema  wanasubiri  kukabidhiwa  rasmi ili kuweza kulizungumzia kwa vyombo vya habari barua na  viongozi wa chama  watapitia katiba yao na kupata mwongozo na kuangalia namna ya  kuziba nafasi hiyo mpaka Uchaguzi  Mkuu  wa  mwaka 2020.
Mbika amesema kuwa kujiengua kwa kada huyo ni pigo kwa chama kwani alikuwa ana mchango mkubwa wa ushawishi na kujenga umoja na mshikamano wa kweli wa ndani na nje ya mkoa

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.