ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 13, 2017

SIJAFA, NINA NGUVU KAMA KIJANA WA MIAKA 20 - DK. MZINDAKAYA.

Dar es Salaam. Mwanasiasa mkongwe na kada wa CCM, Dk Chris Mzindakaya amesikitishwa na watu wanaovumisha taarifa kuwa amefariki na kuwaita ni wapumbavu.

Akizungumza leo akiwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, (JKCI), Mzindakaya amesema afya imeimarika zaidi na ataruhusiwa kuondoka hospitalini hapo wakati wowote.

 Usiku wa kuamkia leo mtandao ya kijamii ilikuwa ikisambaza taarifa potofu za kifo chake.

Baada ya uvumi huo,Dk Mzindakaya alitoa kauli hiyo leo huku akiwahakikishia waandishi kuwa baada ya matibabu, madaktari wamemweleza Afya yake imeimarika mfano wa kijana wa miaka 20.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.